Simba ushindi tuu katika Ligi kuu Vodacom ,Liverpool hoi mara ya 5 ili hali Manchester City yapokonywa tonge mdomoni katika Ligi kuu Uingereza. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, September 23, 2012

Simba ushindi tuu katika Ligi kuu Vodacom ,Liverpool hoi mara ya 5 ili hali Manchester City yapokonywa tonge mdomoni katika Ligi kuu Uingereza.


Simba SC; Juma Kaseja, Nassor Masoud ‘Chollo’, Amir Maftah, Shomari Kapombe, Juma Nyosso, Amri Kiemba, Mwinyi Kazimoto, Ramadhani Chombo ‘Redondo’/Edward, Felix Sunzu, Daniel Akuffo/Boban na Mrisho Ngassa.


Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya soka ya Vodacom Tanzania Bara, Wekundu wa msimbazi Simba SC  wameendeleza wimbi la ushindi baada ya kuilaza mabao 2-1  timu ya Ruvu Shooting ya Pwani, kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.


Shukrani kwake mshambuliaji chipukizi, Christopher Edward aliyeingia kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Ramadhan Chombo ‘Redondo’ kwa kufunga bao la ushindi dakika ya 80 na kuifanya Simba ifikishe pointi tisa baada ya kucheza mechi tatu, nyavu zake zikitikiswa kwa mara ya kwanza leo.


Simba sasa inaendelea kuongoza Ligi Kuu, ikifuatiwa na Azam FC yenye pointi saba, wakati watani wao wa jadi, Yanga wana pointi tatu tu baada ya mechi tatu.  


Ruvu Shooting; Benjamin Haule, Michael Pius, Mau Bofu, George Michael, Said Suzan, Gideon David, Abdulrahman Mussa, Hassan Dilunga, Paul Ndauka/Seif rashid, Hussein Said na Said Dilunga.


Hadi mapumziko, Simba walikuwa tayari mbele kwa bao 1-0, lililowekwa kimiani na mshambuliaji wa kimataifa wa Zambia, Felix Mumba Sunzu Jr. dakika ya 29, akiunganisha krosi ya Nassor Masoud ‘Chollo’.

 Katika dakika ya 45, kipa Benjamin Haule wa Ruvu Shooting alipangua mkwaju wa penalti wa mshambuliaji wa kimataifa wa Ghana, Daniel Akuffor baada ya beki mmoja wa timu hiyo kuunawa mpira kwenye eneo la hatari.



Kipindi cha pili, Ruvu Shooting inayofundishwa na kocha maarufu nchnini, Charles Boniface Mkwasa ilisawazisha bao dakika ya 80, baada ya Seif Rashid kutumia vizuri makosa ya beki Juma Nyosso dakika ya 75.


Seif aliupitia mpira miguuni mwa Nyosso, ambaye alianzishiwa na kipa Juma Kaseja na kutokana na kuchelewa kuamua, akasababisha kilichotokea.


Shukrani wake, chipukizi Edward aliyeifungia bao la ushindi Simba inayofundishwa na Mserbia, Milovan Cirkovick dakika ya 80.



Ratiba ya mechi zijazo Ligi kuu soka Vodacom Tanzania bara.

Septemba 26.
 
Coastal Union v Kagera Sugar[Mkwakwani, Tanga]

Polisi Morogoro v Toto Africans [Jamhuri, Morogoro]

Septemba 28.

Azam v JKT Ruvu [Azam Complex, Dar es Salaam]

Septemba 29.

JKT Oljoro v Mgambo JKT [Sheikh Amri Abeid, Arusha]

Simba v Tanzania Prisons [National Stadium, Dar Es Salaam]

Septemba 30.

Yanga v African Lyon [National Stadium, Dar es Salaam]

Oktoba 1 .

Ruvu Shooting v Mtibwa Sugar [Azam Complex, Dar es Salaam]

Oktoba 3 .

African Lyon v Toto Africans [Azam Complex, Dar es Salaam]

Ruvu Shootings v Kagera Sugar [Mabatini, Pwani], Pwani]

JKT Oljoro v Coastal Union [Sheikh Amri Abeid, Arusha]

Yanga v Simba [National Stadium, Dar es Salaam].




Ligi Kuu Uingereza matokeo ya Leo Septemba 23..




Laurent Koscielny's second half strike saves a point for the Gunners following an impressive display after Manchester City took the lead against the run of play through Joleon Lescott. Mancini's men were unconvincing as Arsenal become the third side to take a point away from the Etihad in their last 32 home league matches.
 
 Manchester city 1-1 Arsenal.


Robin van Persie's late penalty secured Manchester United's first Anfield win since December 2007 against 10-man Liverpool on an emotional afternoon on Merseyside.

The hosts played 51 minutes with 10 men after Jonjo Shelvey's sending-off but still managed to take the lead through Steven Gerrard's volley seconds after the interval.


Man United 2 – 1  Liverpool.



Demba Ba put his rift with Alan Pardew behind him to net the winning goal in Newcastle's 1-0 victory over Norwich on Sunday. 

Tottenham  2 vs 1  QPR.

  



Msimamo wa  Timu za Juu Ligi kuu Uingereza:


1 Chelsea Mechi 5 Pointi 13

2 Man Utd Mechi 5 Pointi 12 

3 Everton Mechi 5 Pointi10

4 WBA Mechi 5 Pointi 10

5 Arsenal  Mechi 5 Pointi  9 

6 Fulham Mechi 5 Pointi 9 

7 Man City Mechi 5 Pointi  9 

Tottenham Mechi 5 Pointi 8

9 West Ham Mechi 5 Pointi 8

10 Newcastle Mechi 5 Pointi 8

11 Swansea Mechi 5 Pointi  7


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad