Kampeni ya Choo ni Nyumba yabaini Kaya Zaidi ya 600 Ngara kukosa Choo Bora. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, July 25, 2018

Kampeni ya Choo ni Nyumba yabaini Kaya Zaidi ya 600 Ngara kukosa Choo Bora.

Mfano wa Choo Bora.

Jumla ya kaya 604 Wilayani Ngara Mkoani Kagera hazina Vyoo Bora kutokana na takwimu zilizo patikana baada ya Kampeni ya Choo ni Nyumba iliyofanyika kwa Usimamizi wa Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo.
Akizungumza na Radio Kwizera Bw Aidan Bahama amesema viongozi wote kuanzia ngazi ya shina mpaka tarafa wafuatilie na kubaini nyumba ambazo hazina vyoo ikiwa ni pamoja na kuwaelimisha wananchi juu ya umuhimu wa choo.

Aidha amewataka viongozi wote kuanzia mabalozi kuorodhesha kaya ambazo hazina choo na kuahidi kuzisaidia familia ambazo hazina uwezo wakujenga choo kutokana na matatizo mbalimbali.

Naye Mratibu wa Kampeni ya kitaifa ya Usafi wa Mazingira wilayani Ngara Bw Mansour Kalokola amewataka watendaji wa vijiji na kata kuandika majina kwenye madaftari yaliyo tolewa kwa ajili ya takwimu ili ziweze kufanyiwa kazi.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad