![]() |
Maafisa Elimu
Kata 22 katika Halmashauri ya Wilaya ya Ngara mkoani Kagera wametakiwa kutumia
pikipiki walizopata kuinua kiwango cha elimu katika kata zao, ili wilaya ipande
kielimu na kufikia nafasi ya kwanza kimkoa na hata kitaifa.
Mkuu wa Mkoa
wa Kagera Brigedia Jenerali Marco Gaguti
ameyasema hayo Septemba 08, 2018 katika ofisi za Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
alipokuwa akiwakabidhi pikipiki 22 kwa Waratibu wa Elimu katika Kata 22 za
Halmashauri hiyo.
Amewambia
Maafisa Elimu hao kuwa yeye kama Mkuu wa Mkoa anapowakabidhi pikipiki hizo
anatarajia kuona ubora wa elimu katika mkoa wa Kagera unaongezeka; na kuogeza
kwamba kuanzia mwaka 2019 mkoa utachukua nafasi ya kwanza katika kufaulu
mitihani ya darasa la saba kitaifa.
“Tumepewa vifaa hivi tuvitunze vifanye kazi
leo, vifanye kazi kesho na siku zote zijazo, ili elimu iendelee kuwa bora siyo
katika mkoa wa Kagera tu, bali katika taifa zima.” Alisisitiza Mkuu huyo wa
Mkoa wa Kagera.
Aidha Serikali
imewakabidhi pikipiki 2,894 Waratibu wa Elimu katika Kata za nchi nzima kwa ajili
ya kuboresha sekta hiyo na zina thamani ya zaidi ya Shilingi Bilioni 8 ukiwa na malengo ya kutembelea na kukagua shule
zilizopo mbali.
|
Post Top Ad
Tuesday, September 11, 2018

RC Kagera alivyo Wamwagia Waratibu wa Elimu Ngara Neema ya Pikipiki.
Tags
# MATUKIO
Sambaza Hii
Chief Editor | Mhariri
Journalist / Chief Editor / Tanzanian Blogger
Simu: 0756830214 / 0620197747 / 0789925630.
Makala Inayofuata
Hifadhi Tano Tarajiwa za Taifa Kagera ni Fursa kwa Wananchi.
Makala Iliyopita
Serikali yakabidhi Pikipiki 22 Maafisa Elimu Ngara Kusimamia Ubora wa Elimu.
Muonekano wa Uwanja wa CCM Kirumba Jijini Mwanza.
AnonymousDec 10, 2019Viongozi Wilayani Kasulu watakiwa Kuimarisha Usalama Katika Korongo la Bolelo.
AnonymousJun 29, 2019Shirika la Ndege la Tanzania Laanza Safari za Afrika Kusini Leo 28/06/2019.
AnonymousJun 28, 2019
Labels:
MATUKIO
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment