![]() |
Mgonjwa akiwa amelalani Ndani.
Mgonjwa huyo
amelazwa kwenye nyumba iliozeeka ambayo iliachwa na mama yake aliyefariki miaka
kadhaa sasa, imejengwa kwa udongo, analala kwenye jamvi la makuti ya migomba
akiwa na blanketi ambalo ni chafu lililoshikana na nyama za mwili wake.
Francisco Kitulu ambaye ni Mwenyekiti wa ukoo
wa ABAVUMU alisema
mgonjwa huyo alitelekezwa na ndugu zake baada ya kuwataka wauze shamba
kupata fedha kumsafirisha hadi hospitali ya Bugando lakini wao walikataa
na kujiingiza kwenye matibabu ya waganga wa kieyeji.
Alisema
sehemu ya shamba iliyouzwa waliitafuna kwa kunywa pombe na kiasi kingine
kumpelekea mganga wa miti shamba lakini hali ni mbaya kwani sehemu ya nyonga
inaonekana mifupa baada ya nyama za mwili kushmbuliwa na wadudu.
|
![]() |
Waandishi wa
habari wakiwa nje ya nyumba alikolala Mgonjwa.
Mwenyekiti
wa kijiji cha Murukukumbo Simon John
alipoulizwa kuhusu mgonjwa uyo alisema anazo taarifa zake lakini alijua
wanaukoo na familia wanamuuguza hivyo hakuwai kupata malalamiko ya mgonjwa
kutelekezwa.
Majirani na
watu wengine katika kijiji hicho walisema tangu kuugua kwake kijana
huyo Gwassa Jacob hawakushirikishwa
na ndugu zake au viongozi ili apelekwe hospitali kwani wangetoa michango
yao kumpatia chakula na mahitaji mengine.
|
![]() |
Gwassa Jacobo aliondoa kijiji cha Mulukuumbo
akielekea wilaya ya Karagwe Mkoani Kagera, kutafuta maisha na kumpata mke
aliyezaa naye watoto wawili mmoja wao ana umri wa miaka minane alipata
naye ajali mwezi februari kweye shimo la choo na kupata majeraha ya kawaida.
Inasemekekana
wakati akipata matibabu katika hospitali ya mkoa wa Kagera alijitokeaza
msamalia mwema abaye hakujulikana aliyemchukua mtoto wake wa kiume
kwenda kuishi naye akidai atamsomesha shule ya msingi.
Oliva Niyonzima ambaye ni Mtawa kutoka Shirika
la Masister wa Francisco wa Mt. Bernadetha Jimbo Katoliki la Rulenge Ngara
alifika ndani ya nyumba alikolala mgonjwa huyo baada ya kumfunua alikuta
mwili ukitoka wadudu na harufu kali.
Niyonzima aliwaomba Wananchi kujawa na
moyo wa huruma kujitokeza kumaiidia kwa kumuondoa kwenye nyumba allikolazwa na
kumpeleka sehemu yenye usalama ili asijekudhuliwa na mbwa wa usiku.
Waandishi wa
habari walioungana na Sister Oliva
Niyonzima alishauri wananchi na viongozi pia wanaukoo kumfuatilia mgonjwa
huyo na kumpatia huduma kama chakula na kufanya usafi wa mwili wake kisha
kumfikisha Hospitali.
|
No comments:
Post a Comment