Odinga: Ni siku ya kihistoria Kenya na kwa Afrika. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Friday, September 01, 2017

Odinga: Ni siku ya kihistoria Kenya na kwa Afrika.

Pichani ni Wafuasi wa kiongozi wa upinzani Raila Odinga jijini Nairobi wamekuwa barabarani wakisherehekea hatua ya Mahakama kubatilisha Matokeo ya Uchaguzi wa Urais leo September 01,2017.

Mgombea wa Muungano wa Nasa, Raila Odinga.

Kufuatia Mahakama ya Juu nchini Kenya kufutilia mbali matokeo ya uchaguzi mkuu wa urais uliofanyika mapema mwezi uliopita wa nane katika uamuzi kuhusu kesi iliwasilishwa na muungano wa upinzani National Super Alliance ,Mgombea urais wa upinzani  Bw.Raila Odinga amesema leo September 01,2017  ni siku ya kihistoria kwa Kenya na kwa Afrika.

"Tulisema tangu awali kwamba safari yetu ya Canaan haiwezi kuzuiwa. Siku ya tarehe 8 Agosti tulivuka mto Jordan."

Bw Odinga amesema upinzani hauna imani kwamba tume ya sasa ilivyo inaweza kuandaa uchaguzi huru na wa haki.

Wafuasi wa kiongozi wa upinzani Raila Odinga jijini Nairobi wamekuwa barabarani wakisherehekea hatua ya Mahakama kubatilisha Matokeo ya Uchaguzi wa Urais leo September 01,2017.



Hii ni mara ya kwanza katika historia ya Taifa hilo kwa Mahakama ya Juu kufuta matokeo ya uchaguzi na inaweka rekodi mpya katika historia ya uchaguzi barani Afrika ndani ya mfumo wa vyama vingi.

Katika uchaguzi uliopita,Bw. Odinga alienda mahakamani kupinga matokeo lakini Mahakama hiyo ilitupilia mbali hoja zake na kuridhia matokeo yaliyompa ushindi Rais Kenyatta.

Katika uchaguzi wa Agosti 8,2017,Bw. Kenyatta alitangazwa mshindi kwa kupata kura 8,203,290 sawa na asilimia 54.27, huku mpinzani wake Bw.Odinga akipata kura 6,762,224 sawa na asilimia 44.74.

Kwa uamuzi uliotolewa na mahakama, uchaguzi mwingine unapaswa kufanyika katika kipindi cha siku 60. Iwapo ushindi wa Kenyatta ungeidhinishwa angepaswa kuapishwa Septemba 12.

Kumekuwa na shamrashamra katika mitaa mbalimbali ya Nairobi na Mombasa kushangilia uamuzi huo, huku Odinga akiwa na wanasiasa wenzake wamepongeza wakisema watatoa taarifa zaidi baadaye.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad