Chanzo cha Diwani kurushiwa mishale wilayani Karagwe,Kagera. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, August 31, 2017

Chanzo cha Diwani kurushiwa mishale wilayani Karagwe,Kagera.

Jeshi la polisi kwenye Wilaya ya Karagwe limewatia mbaroni watuhumiwa waliohusika kwenye shambulio la mikuki lililofanyika juzi dhidi ya Mkuu wa Wilaya hiyo,Bw.Godfrey Mheruka na Diwani wa kata ya Nyakahanga Mhe.Charles Bechumila na inasemekana kuwa washambuliaji hao ni watoto na walinzi wa aliyetoa agizo la shambulio hilo.

Kwa mujibu wa Mkuu huyo wa Wilaya shambulio hilo linatokana na mgogoro wa ardhi uliopo kati ya wananchi na mtu anayejulikana kwa jina la Kamiyanda ambaye amejimilikisha ekari 152 za eneo hilo na pindi diwani alipoitisha mkutano wa kijiji bwana huyo alihisi ni mbinu za kumtoa yeye na hivyo kuwatuma watu hao kwa ajili ya shambulio hilo.

Diwani Bechumila aliyejeruhiwa kutokana na tukio hilo alichomwa mikuki minne maeneo ya shingoni, ubavuni, kifuani na kwenye paja na mpaka sasa bado anapatiwa matibabu katika Hospitali ya Nyakahanga.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad