Taswira Picha Waislam kote duniani wanaadhimisha sherehe za Eid el-Hajj. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Friday, September 01, 2017

Taswira Picha Waislam kote duniani wanaadhimisha sherehe za Eid el-Hajj.

Manila, Ufilipino : Mvulana mdogo anaonekana akiwa amesimama katika umati wa waumini katika ibada ya Eid el-Hajj.

Waislam kote duniani wanasherehekea sherehe za Idd el-Hajj, zinazofanyika wakati wa Hija inayofanyika kila mwaka mjini Mecca.

Sherehe hiyo ambayo pia hufahamika kama sherehe ya kuchinja au kutoa kafara, ni moja kati ya sherehe kubwa za kiislam ikiwa ni kutekeleza nguzo ya mwisho katika nguzo 5 za kiimani katika dini ya kiislam.

Ni kumbu kumbu ya kujitolea kwa utashi kwa Abraham kumtoa kafara mwanae kwa Mungu na wakati wa sherehe hii waislam hutoa kafara wanyama.
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk Hussein Mwinyi, akihutubia waumini wa kiislamu.

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Dk Hussein Mwinyi, leo September 01,2017 amewaongoza waumini wa Kiislamu katika kusherehekea sikukuu ya Eid El Hajj ambayo ni maarufu kama ‘Eid ya Kuchinja’.

Waziri Mwinyi amesisitiza suala la amani kwa Watanzania wote huku akikazia maneno ya Mufti Zuberi aliyokuwa ameyatamka ili waumini waweze kubadilika, akimaanisha kuondokana na dhana zote potofu zisizokuwa na manufaa katika kulijenga taifa chini ya Rais Magufuli na serikali yake.

Hafla hiyo imefanyika jijini Dar es Salaam kwenye viwanja vya Masjid Taqwa, Ilala-Bungoni jijini Dar es Salaam, kuanzia saa 1:30 asubuhi ambapo Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa na Mufti Mkuu wa Tanzania, Abubakar Zuberi, na viongozi wengine wamehudhuria sherehe hizo.
 Mufti Mkuu wa Tanzania, Abubakar Zuberi akisoma ujumbe wa Eid El Hajj kwa Watanzania.
Baadhi ya Waislam waliofika kwenye sherehe hizo.

Akizungumza katika viwanja hivyo, Mufti Mkuu wa Tanzania, Abubakar Zuberi amesema kuwa anawatakia Waislamu kote nchini na wananchi kwa jumla sikukuu njema ya Eid El Hajj ili kila mmoja aisherehekee kwa utulivu na mshikamano.

Amewataka pia walimu kote nchini wa shule za Kiislamu za madrasa kufanya jitihada kubwa ya kuhakikisha wanawaelimisha wanafunzi wao ili waweze kuwa na maadili mema na si kuwapatia elimu ya dini yao tu, bali wafundishwe pia masomo mbalimbali ili kuwawezesha kuwa na maadili mema na utaalam unaotakiwa katika maisha yao ya baadaye na kuwa viongozi bora.

Mufti alitoa miezi sita kwa taasisi iliyokuwa na jukumu la kuwasafirisha mahujaji kwenda Makka na kushindwa kufanya hivyo, irudishe fedha ilizokuwa imezichangisha kutoka kwa waumini waliotegemea kwenda huko.

Alisema waumini hao wataweza kwenda kuhiji huko Makka mwaka kesho na kwamba uongozi wake utahakikisha tatizo kama hilo haliwezi tena kujitokeza na kuathiri safari za mahujaji.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad