VPL 2016/2017: Yanga SC yashindwa kutamba mbele ya African Lyon. - Mwana Wa Makonda
cV7ufzj

Muhtasari

X-BET

MAIN-

Post Top Ad

cV7ufzj

Friday, December 23, 2016

demo-image

VPL 2016/2017: Yanga SC yashindwa kutamba mbele ya African Lyon.

.com/simgad/
1

Ligi Kuu Soka Vodacom Tanzania bara msimu huu 2016/2017 imeendelea leo December 23,2016 kwa Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Yanga SC kucheza dhidi ya African Lyon katika uwanja wa Uhuru Dar es Salaam.

Kabla ya mchezo wa leo, African Lyon kucheza na Yanga SC, rekodi zilikuwa zinasomeka kuwa kwa mechi 7 zilizopita, African Lyon hajawahi kumfunga Yanga SC huku akiwa amekubali kufungwa mara sita na kutoa sare mechi moja pekee toka tarehe 27/10/2010.

2

Haidi dakika 90 za mchezo ,Yanga SC leo wameshindwa kutamba mbele ya African Lyon na kujikuta wakilazimishwa sare ya kufungana goli 1-1.

 Venance Ludovic ndio aliipatia goli la kwanza African Lyon dakika ya 59, kabla ya Amissi Tambwe kuisawazishia Yanga SC goli dakika ya 74.

Ligi hiyo itaendelea tena Hapo kesho Jumamosi December 24,2016 kwa mechi zifuatazo hapa chini:-
  15658690_1327373677302539_1665363343_o

Yanga SC inaendelea kusalia katika nafasi ya pili ikiwa na pointi zake 37 pointi moja nyuma ya Simba SC ambayo itacheza kesho December 24 dhidi ya JKT Ruvu.

Endapo Simba SC itashinda mchezo huo itaongeza gap la pointi hadi kuwa nne kwa sababu itakuwa imefikisha pointi 41 huku Yanga SC ikiwa na pointi 37, lakini kama Simba SC itafungwa bado itaendelea kuongoza kwa pointi moja wakati ikitoka sare itakuwa kileleni kwa pointi mbili.

 
Na huu ni Msimamo wa Ligi kuu Ulivyo kwa sasa.

15658862_1327373780635862_858121657_o

15658267_1327373673969206_1409681847_o

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad

Contact Form

Name

Email *

Message *