|
Wekundu wa
Msimbazi ,Simba SC imepaa kileleni mwa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kwa
pointi saba zaidi ya wapinzani Azam FC na Yanga SC katika mbio za ubingwa, kufuatia
ushindi wa 2 - 0 dhidi ya Coastal Union Uwanja wa Mkwakwani, Tanga jioni ya leo,March
19, 2016.
Mchezaji,Danny Lyanga
aliifungia Simba SC goli la kwanza dakika ya 39 kipindi cha kwanza kisha Hamis Kiiza
akamaliza kazi dakika ya 51 na kupeleka shangwe kwenye mtaa wa Msimbazi.
Simba SC
sasa inafikisha pointi 57, baada ya kucheza mechi 24, wakifuatiwa na mabingwa
watetezi, Yanga SC wenye pointi 50 sawa na Azam FC baada ya timu zote hizo kucheza
mechi 21.
Coastal
Union iliyozifunga Yanga SC 2 - 0 na Azam FC 1- 0 Uwanja wa Mkwakwani, kipigo cha leo
kinawafanya wabaki na pointi zao 19 baada ya kucheza mechi 24 na kuendelea
kuburuza mkia katika Ligi Kuu ya timu 16.
Huko Songea,
Majimaji FC imeinyuka Mbeya City 2-1 na kushika Nafasi ya 8 wakiwa na Pointi 27
huku Mbeya City wakiwa Nafasi ya 11 na wana Pointi 24 Wakati mchezo wa Stand
United na Ndanda FC wakitoka sare ya bao
1-1.
LIGI KUU
VODACOM 2015/2016 – RATIBA.
Jumapili
Machi 20,2016.
African
Sports v Tanzania Prisons
Jumatatu
Machi 21,2016.
Mgambo JKT v
Toto Africans
Alhamisi
Machi 24,2016.
African
Sports v Toto Africans
|
No comments:
Post a Comment