TAZAMA PICHA:-Ni Maombi ya Kumuombea Rais Magufuli na Taifa January 13, 2016 Jijini Mwanza. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, January 14, 2016

TAZAMA PICHA:-Ni Maombi ya Kumuombea Rais Magufuli na Taifa January 13, 2016 Jijini Mwanza.

Viongozi mbalimbali wa dini wakiwa katika picha ya pamoja na Mgeni Rasmi Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Magesa Mulongo (wa pili kushoto walioshikilia bendera), katika Maombi ya Kumuombea Rais Magufuli na Taifa yaliyofanyika jana January 13,2016,Jijini Mwanza.

Umoja wa Makanisa Jijini Mwanza kwa kushirikiana na Umoja wa Maaskofu kutoka Jijini Dar es salaam jana January 13,2015 ulifanya Mamombu Maalumu ya Kumuombea Rais wa wa awamu ya tano ya Jamhuri ya Muungani wa Tanzania Mhe.Dkt.John Pombe Magufuli pamoja na Wasaidizi wake.

Maombi hayo yalifanyika katika Uwanja wa Furahisha Manispaa ya Ilemela Mkoani Mwanza na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo viongozi wa Serikali na Dini huku pia wananchi wakijumuika pamoja na waumini wa dini mbalimbali katika maombi hayo.
Viongozi mbalimbali wa dini wakiwa katika picha ya pamoja na Mgeni Rasmi Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Magesa Mulongo (Wa tatu kushoto) katika Maombi ya Kumuombea Rais Magufuli na Taifa yaliyofanyika jana Jijini Mwanza.


Kulia ni Mwenyekiti Msaidizi wa Umoja wa Makanisa Jijini Mwanza Zenobius Isaya akiwa katika Maombi ya kumuombea Rais Magufuli, wasaidizi wake pamoja na Taifa yaliyofanyika jana Jijini Mwanza.

Mgeni Rasmi Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Magesa Mulongo akizungumza katika Maombi ya kumuombea Rais Magufuli, wasaidizi wake pamoja na Taifa yaliyofanyika jana Jijini Mwanza.

 Mgeni Rasmi katika maombi hayo alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Magesa Mulongo ambae katika hotuba yake, aliwasihi Watanzania wote kuendelea kuliombea Taifa ili kuondokana na vikwazo mbalimbali ambapo alidokeza kuwa kupitia maombi kama yaliyofanyika jana, migogoro mbalimbali ikiwemo ya kisiasa kama iliyopo Zanzibar itamalizika.

Viongozi mbalimbali wakiwemo Mwenyekiti wa Umoja wa Makanisa Jijini Mwanza Askofu Charles Sekelwa, Makamu wake Zenobius Issaya pamoja na Kiongozi wa Kundi la Maaskofu kutoka Jijini Dar es salaam la Good News For all Ministry Askofu Dr.Charles Gadi pamoja na viongozi wengine wa dini kutoka mikoa mbalimbali nchini waliliombea Taifa na kuhimiza utuliza nchini.

Wasaidizi wa wa Rais Maguguli ambao ni pamoja na Makamu wa Rais Mhe.Samia Suluhu, Waziri Mkuu Mhe.Kassim Majaliwa, Jaji Mkuu Mhe.Othman Chande, Spika wa Bunge Mhe.Job Ndugai, Mawaziri pamoja na viongozi wengine wa Serikali wa awamu ya tano waliombewa ili kuliongoza vema taifa kwa kuendana na kasi ya Rais Magufuli.

Pamoja na mambo mengine, maombi hayo yalijumuisha toba kwa taifa, kumuomba Mungu kukomesha mauaji ya Vikongwe na watu wenye ulemavu wa ngozi pamoja na kuombea taifa mvua zisizo na madhara.

Maombi ya kumuombea Rais Magufuli, wasaidizi wake pamoja na Taifa yaliyofanyika jana Jijini Mwanza.TAZAMA PICHA ZAIDI KWA KUBOFA HAPA NA BINAGI MEDIA GROUP

Papo kwa Papo >>>> Pata Picha, Habari za  Siasa, Kijamii, Biashara, Muziki na Michezo na Nyingine kwa kujiunga  na mimi hapa…..FACEBOOK , TWITTER INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad