UCHAGUZI MKUU ZANZIBAR 2015:- Ifahamu sababu ya ZEC Kufutwa Matokeo ya uchaguzi . - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, October 29, 2015

UCHAGUZI MKUU ZANZIBAR 2015:- Ifahamu sababu ya ZEC Kufutwa Matokeo ya uchaguzi .

uchaguzi

Pichani kushoto ni Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha.

Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha ametangaza kufuta matokeo ya Uchaguzi  mkuu visiwani Zanzibar, uliofanyika Oktoba 25, 2015.

Jecha amesema kuwa, ZEC imefuta matokeo ya uchaguzi kutokana na kukiukwa kwa sheria na taratibu mbalimbali za uchaguzi wakati wa utekelezaji wa zoezi hilo.

Uchaguzi huo utarudiwa baada ya siku 90.

Amesema baadhi ya makamishna wa tume hiyo, badala ya kutekeleza majukumu yao inavyotakiwa kikatiba "wamekuwa ni wawakilishi wa vyama vyao".

Tangazo la mwenyekiti huyo limetolewa huku hali ya wasiwasi ikiendelea kutanda visiwani humo.

Siku moja baada ya uchaguzi kufanywa,October 26,2015 mgombea wa chama cha upinzani cha Civic United From (CUF) Seif Sharif Hamad alijitangaza kuwa mshindi, hatua iliyokemewa na chama cha CCM ambacho mgombea wake Dkt Ali Mohamed Shein amekuwa rais wa visiwa hivyo muhula unaomalizika.

Tume ya uchaguzi visiwani Zanzibar - ZEC pia ilishutumu hatua ya mgombea huyo.

 Kabla ya kufutiliwa mbali kwa matokeo ya uchaguzi, tume hiyo ya uchaguzi ilikuwa imetangaza matokeo ya majimbo 31 kati ya majimbo 54 visiwani humo.

Hayo yakijiri Tume ya Taifa ya Uchaguzi Tanzania - NEC inaendelea kutoa matokeo ya uchaguzi wa URAIS.  Kufikia sasa imetoa matokeo ya majimbo 155 kati ya majimbo 264.

TAARIFA ZAIDI HAPA CHINI

Papo kwa Papo >>>> Pata Picha, Habari za  Siasa, Kijamii, Biashara, Muziki na Michezo na Nyingine kwa kujiunga  na mimi hapa…..FACEBOOK , TWITTER INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.  

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad