TASWIRA PICHA:-Zoezi la kugawa Chakula laendelea katika Kambi ya Wakimbizi Nyarugusu wilayani Kasulu mkoani Kigoma. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Tuesday, September 08, 2015

TASWIRA PICHA:-Zoezi la kugawa Chakula laendelea katika Kambi ya Wakimbizi Nyarugusu wilayani Kasulu mkoani Kigoma.


Wakimbizi kutoka nchini Burundi  walioko katika kambi ya Nyarugusu wakiwa wamebeba shehena ya unga wa mahindi jana, muda mfupi baada ya kugawiwa chakula hicho Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia chakula (WFP), lililoweka kituo chake katika kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu wilayani Kasulu, mkoani Kigoma.


Byesige Josephat (anayemimina mafuta) na Hezron Mtangirwa(kushoto), wakimbizi kutoka Burundi waliohifadhiwa katika kambi ya Wakimbizi ya Nyarugusu wakipima mafuta ili waweze kuyagawa kwa wakimbizi wenzao jana ,baada ya kugawiwa mafuta na Shirika la Umoja wa Mataifa, linaloshughulikia chakula (WFP), ambalo lina kituo chake katika kambi ya Nyarugusu iliyoko wilayani Kasulu mkoani Kigoma.

Idadi ya waomba hifadhi kutoka nchini Burundi katika kambi ya wakimbizi ya nyarugusu wilayani Kasulu mkoani Kigoma imeendelea kuongezeka ambapo sasa imefikia watu elfu 91 na 661.



Akiongea na Radio Kwizera, mkuu wa makazi Kambini Nyarugusu, Bw Sospeter Boyo amesema kuwa idadi ya waomba hifadhi hao inazidi kuongezeka kila siku,ambapo  mpaka sasa wananaendelea kupokea waomba hifadhi na kuwa kasi ya kuingia kwa saa ni ndogo ukulinganisha na mwezi wa sita na wa saba, ambapo kwa sasa wanapokea waomba hifadhi chini ya 100.



Aidha Bw Boyo amesema kuwa kwa mujibu wa waomba hifadhi hao wanakimbia nchini mwao kutokana na mauaji ya chinichini yanayo endelea nchini mwao licha ya uchaguzi mkuu kumalizika nchini Burundi.

Kinamama wakimbizi toka Burundi wakipata mgao wao wa unga unaotolewa kwa wakimbizi wanaohifadhiwa katika Kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu iliyoko wilayani Kasulu mkoani Kigoma.  Serikali kwa kushirikiana na Mashirika ya Kimataifa imeendelea kuhakikisha kuwa wakimbizi hawa toka Burundi wanapata chakula cha kutosha kwa ajili ya mahitaji yao.

Mkimbizi Irene Ntibelenda (katikati) akiwa pamoja na ndugu yake Sengiyu Mvajeme (kulia) baada ya kupokea mgao wa chakula unaotolewa na  Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia chakula (WFP), lililo  na Kituo chake katika kambi ya Nyarugusu iliyopo wilayani Kasulu, mkoani Kigoma. Kushoto ni mtoto wake aitwaye Nsengiyumva Idiphonce.
Mkimbizi kutoka nchini Burundi, Josef Ntukugurya akifunga shehena ya unga wa mahindi jana, muda mfupi baada ya kupokea unga huo kutoka kwa Shirika la Umoja wa Mataifa, linashughulikia chakula (WFP), lililoweka kituo chake katika kambi ya Nyarugusu iliyopo wilayani Kasulu, mkoani Kigoma . 

Sehemu ya shehena ya chakula ukiwepo unga wa mahindi na mafuta ya kupikia ikiwa katika ghala la kuhifadhia chakula lililopo katika kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu iliyoko wilayani Kasulu mkoani Kigoma.  Chakula hiki hutolewa na Jumuiya ya Kimataifa kama kupitia Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia chakula (WFP) ili kusaidia wakimbizi wanaohifadhiwa hapa nchini.

(PICHA NA KITENGO CHA MAWASILIANO YA SERIKALI – WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI).


Papo kwa Papo >>>> Pata Picha, Habari za  Siasa, Kijamii, Biashara, Muziki na Michezo na Nyingine kwa kujiunga  na mimi hapa…..FACEBOOK , TWITTER INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad