![]() |
Mgombea
Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA),
Mh. Edward Lowassa, akionyesha mfano wa funguo kwa umati wa wananchi wa
Singida, waliofurika kwa wingi kwenye Uwanja wa Peoples, Mjini humo leo
Septemba 12, 2015.
Mgombea huyo
wa Urais wa vyama vinavyounda UKAWA Mh.Edward Lowassa amesema akichaguliwa kuwa rais hatakuwa na sababu ya
kutegemea misaada kutoka nje kutekeleza
ahadi anazotoa na sera zilizoko kwenye ilani ya UKAWA badala yake atasimamia vizuri rasilimali zilizopo kwani
zinatosha kutatua matatizo ya
watanzania.
Baada ya
kumaliza kazi ya kufikisha ujumbe wa mabadiliko kwa wananchi wa mkoa wa Dodoma
ambao ni ngome na pia makao makuu ya CCM kwa mafanikio makubwa Mh.Lowasa anaingia kwa kishindo katika mkoa
wa Singida na kupokelewa na umati wa wananchi wakiwa na matumaini
makubwa ya kupata mabadiliko ya maisha yao kupitia ukawa chini ya
Mh.Lowasa,ambaye amewaomba kumpa nafasi ya kushughulikia kero zao kwani anazijua na
asilimia kubwa ufumbuzi wake uko
ndani ya uwezo wake.
Mh.Lowasa
ambaye awali amefanya mikutano katika wilaya ya Manyoni,Ikungi na Singida mjini
anasema kupitia sera zilizoko kwenye ilani ya UKAWA na uwezo mkubwa wa viongozi
na watendaji wana kila sababu ya
kubadilisha maisha ya watanzania kwa muda mfupi
na kwa ufanisi mkubwa...Habari Na:-itv.co.tz/news
|
Saturday, September 12, 2015

Home
SIASA
KAMPENI UKAWA 2015:-Picha zaidi wakati LOWASSA anaingia kwa kishindo katika mkoa wa Singida na kupokelewa na umati wa Wananchi wakiwa na matumaini makubwa ya kupata mabadiliko ya maisha yao.
KAMPENI UKAWA 2015:-Picha zaidi wakati LOWASSA anaingia kwa kishindo katika mkoa wa Singida na kupokelewa na umati wa Wananchi wakiwa na matumaini makubwa ya kupata mabadiliko ya maisha yao.
Tags
# SIASA
Sambaza Hii
Chief Editor | Mhariri
SIASA
Labels:
SIASA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Kuhusu Mwandishi
Journalist / Chief Editor / Tanzanian Blogger
Simu: 0756830214 / 0620197747 / 0789925630.
No comments:
Post a Comment