Liverpool
leo Octoba 04,2014,jioni imepata ahueni na bila shaka kocha Brenden Rodgers
atapumua leo. Hiyo inafuatia ushindi wa mabao 2-1 West Bromwich Albion Uwanja
wa Anfield.
Shukrani kwao, wafungaji wa mabao hayo, Adam Lalana dakika ya 45 na Jordan
Henderson dakika ya 61, wakati bao pekee la WBA lilifungwa na Saido Berahino
kwa penalti dakika ya 56.
Katika mechi nyingine za Ligi Kuu ya England jioni ya leo Octoba 04,2014, Hull
City imeifunga 2-0 Crystal Palace, mabao ya Mohamed Diame dakika ya 61 na
Nikica Jelavic dakika ya 89.
Leicester City imetoka 2-2 na Burnley. Mabao ya Leicester yamefungwa na Jeffrey
Schlupp dakika ya 34 na Riyad Mahrez dakika ya 41, wakati ya Burnley yamefungwa
na Michael Kightly dakika ya 39 na Ross Walace dakika ya 90.
Swansea City
imetoka sare ya 2-2 na Newcastle United, mabao yake yakifungwa na Wilfried
Bonny dakika ya 17 na Routledge dakika ya 50, huku ya wapinzani wao yakifungwa
na Papiss Cisse dakika ya 43 na 75.
Sundeland imeichapa 3-1 Stoke City, mabao yake yakitiwa kimiani na Cannor
Wickham dakika ya nne, Steven Fletcher dakika ya 23 na 79, wakati bao la
kufutia machozi la wapinzani wao limefungwa na Charlie Adam dakika ya 15.
|
No comments:
Post a Comment