VIDEO:Kocha Mpya wa Bayern Munich, Pep Guardiola akiifunga timu yake ya zamani, FC Barcelona mabao 2-0 katika mchezo wa kirafiki mjini Munich,Ujerumani. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, July 25, 2013

VIDEO:Kocha Mpya wa Bayern Munich, Pep Guardiola akiifunga timu yake ya zamani, FC Barcelona mabao 2-0 katika mchezo wa kirafiki mjini Munich,Ujerumani.

Mchezaji Philip Lahm (katikati) alifunga bao la kwanza la Bayern Munich wakati  FC Barcelona  wakifungwa mabao 2-0 katika mchezo wa kirafiki mjini Munich hapo jana usiku (Julai 24,2013).

Kocha Mpya wa Bayern Munich, Pep Guardiola ameifunga timu yake ya zamani, FC Barcelona mabao 2-0 katika mchezo wa kirafiki mjini Munich hapo jana usiku (Julai 24,2013).

Nahodha wa FC Barcelona, Lionel Messi alicheza hovyo  kipindi cha kwanza cha mchezo huo akatolewa  wakati  FC Barcelona  wakifungwa mabao 2-0 katika mchezo wa kirafiki mjini Munich hapo jana usiku (Julai 24,2013).

Goli la Pili la mchezaji  Mario Mandzukic  wakati Bayan Munich ilipoiburuza FC Barcelona  mabao 2-0  katika mchezo huo wa kirafiki mjini Munich hapo jana usiku (Julai 24,2013).

Wachezaji Thiago (kushoto) na Boateng (kulia) wa Bayan Munich  wakimdhibiti  Nahodha wa FC Barcelona, Lionel Messi katika mchezo huo wa kirafiki mjini Munich hapo jana usiku (Julai 24,2013).

Frank Ribery akipambana na Marc wa FC Barcelona  katika mchezo huo wa kirafiki mjini Munich hapo jana usiku (Julai 24,2013).

Kocha Guardiola wa  Bayan Munich akionekana mwenye furaha kwa  kuwa na kikosi kizuri  wakati Bayan ilipoiburuza FC Barcelona  mabao 2-0  katika mchezo huo wa kirafiki mjini Munich hapo jana usiku (Julai 24,2013).


Kocha Mpya wa Bayern Munich, Pep Guardiola ameifunga timu yake ya zamani, FC Barcelona mabao 2-0 katika mchezo wa kirafiki mjini Munich hapo jana usiku (Julai 24,2013).

Katika Mchezo huo wa Ziara, FC Barcelona iliyokuwa bila Kocha wao mpya Gerardo Martino na pia Mchezaji mpya Neymar na mihimili yao, Xavi na Andres Iniesta, Pep Guardiola alitumia Mfumo mpya kwa Bayern wa kutokuwa na Straika anaetambulika huku akimchezesha Kepteni wao, Philipp Lahm, ambae amezoeleka kama Fulbeki wa kulia, kama Kiungo Mshambuliaji huku nyuma yake akiwepo Kiungo wao mpya Thiago Alcantara.

Mchezaji Philipp Lahm alifunga bao la kwanza dakika ya 14 na timu zikaenda kupumzika matokeo ya 1-0, kabla ya Bayern kupata bao la pili dakika ya 87 lililofungwa Mario Mandzukic.

Kikosi cha Bayern Munich kilikuwa: Neuer/Starke dk46, Rafinha, Dante/Van Buyten dk59, Boateng, Alaba, Thiago, Lahm/Gustavo dk59, Kroos, Ribery, Robben/Shaqiri dk46 na Muller/Mandzukic dk46.


FC BarcelonaPinto/Oier dk46, Montoya/Kiko dk46, Bartra/Gomez dk46, Mascherano/Planas dk46, Adriano/Patric dk46, Song/Espinosa dk46, Sergi Roberto/Ilie dk46, Dos Santos/Quintilla dk46, Tello/Joan Roman dk46, Messi/Dongou dk46 na Alexis/Dani Nieto dk46.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad