Rais
Kikwete akisalimiana na Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe Mohamed Chande Othman ambaye
pia yuko mkoani Kagera kwa ziara ya kikazi.
|
Rais
Kikwete akisalimiana na Mstahiki Meya wa Bukoba Mhe Anatory Amani.
|
Vijana
wa Skauti wa Bukoba wakimlaki Rais Kikwete mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege
wa Bukoba jana(Julai 24,2013) tayari kuanza ziara ya kikazi ya siku sita mkoani
humo.
|
Kijana
wa Skauti akipiga saluti kuomba kumvisha skafu Rais Kikwete.
|
Rais Kikwete
akivishwa skafu.
|
Rais
Kikwete akisalimiana na Waziri wa Ujenzi Dkt John Pombe Magufuli. Kushoto ni
Waziri wa Maji Profesa Jumanne Maghembe.
|
Rais
Kikwete akisalimiana na Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo.
|
Rais
Kikwete akisalimiana na Viongozi na Wananchi wa Mkoa wa Kagera waliofika
uwanjani kumlaki.
|
Rais Kikwete
akisalimiana na Mkuu wa JKT.
|
Rais
Kikwete akiangalia ngoma za utamaduni mara baada ya kuwasili katika uwanja wa
ndege wa Bukoba jana(Julai 24,2013) tayari kuanza ziara ya kikazi ya siku sita
mkoani humo.
|
Ngoma
ya Kihaya ikimlaki Rais Kikwete mjini Bukoba
mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Bukoba jana(Julai 24,2013)
tayari kuanza ziara ya kikazi ya siku sita mkoani humo.
|
Sehemu
ya viongozi waliohudhuria sherehe ya kuweka jiwe la msingi la ukarabati na
upanuzi wa uwanja wa ndege wa Bukoba jana(Julai 24,2013).
|
Viongozi
wa dini Mkoani Kagera wakiwa bega kwa bega kwenye sherehe hizo za kuweka jiwe
la msingi la ukarabati na upanuzi wa uwanja wa ndege wa Bukoba jana(Julai
24,2013).
|
Waziri
wa Uchukuzi Dkt Harrison Mwakyembe akimkaribisha Rais Kikwete kuongea na
wananchi kabla ya kuweka jiwe la msingi la ukarabati na upanuzi wa uwanja wa
ndege wa Bukoba.
|
Rais
Kikwete akiongea na wananchi kabla ya kuweka jiwe la msingi katika ukarabati na
upanuzi wa uwanja wa ndege wa Bukoba.
|
Rais Kikwete
akipata maelezo kabla ya kuweka jiwe la msingi katika ukarabati na upanuzi wa
uwanja wa ndege wa Bukoba.
|
Rais Kikwete
akifunua kitambaa kama ishara ya kuweka
jiwe la msingi katika ukarabati na upanuzi wa uwanja wa ndege wa Bukoba
jana (Julai 24,2013).
|
Hapa Rais
Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na wadau baada ya kuweka jiwe la msingi
katika ukarabati na upanuzi wa uwanja wa ndege wa Bukoba.
|
Rais Kikwete
akisalimiana na Mhashamu Methodius Kilaini, Askofu Msaidizi wa Jimbo la Bukoba.
|
Sehemu ya
uwanja wa ndege wa Bukoba unaokarabatiwa na kupanuliwa kwa Hivi sasa
ukionekana.
|
Baada ya
Shughuli za Uwanjani ,Rais Kikwete aliwasili Kufungua jengo la kitega uchumi la
Chama Kikuu cha Ushirika (KCU Ltd) mjini Bukoba Pia.
|
Rais Kikwete
akisalimiana na wanachama wa KCU alipowasili jana (Julai 24,2013)Kufungua jengo
la kitega uchumi la Chama Kikuu cha Ushirika (KCU Ltd).
|
Rais Kikwete
akisalimiana na wananchi wa Mjini wa Bukoba waliofurika kushuhudia ufunguzi wa jengo la kitega uchumi la Chama Kikuu cha
Ushirika (KCU Ltd).
|
Mwenyekiti
wa Bodi ya KCU (1990)LTD,Bw. John Binushu
akimkaribisha Rais Kikwete Kufungua jengo la kitega uchumi la Chama
Kikuu cha Ushirika (KCU Ltd) hapo jana(Julai 24,2013).
|
Sehemu ya
umati wa wananchi kwenye ufunguzi wa jengo hilo.
|
Ni muonekano
wa Jengo la kitega uchumi la Chama Kikuu cha Ushirika (KCU Ltd) lililopo mjini
Bukoba.
|
Rais Kikwete
akipokea risala toka kwa Mwenyekiti wa Bodi ya KCU (1990)LTD ,Bw.John Binushu huku Pembeni yake ni Mkuu wa Mkoa wa Kagera Bw.Fabian Masawe.
|
Rais Kikwete
akipokea zawadi ya kahawa toka kwa Mwenyekiti wa Bodi ya KCU (1990)LTD ,Bw.John
Binushu.
|
Rais Kikwete
akifunua kitambaa kama ishara ya Kufungua rasmi jengo la kitega uchumi la Chama
Kikuu cha Ushirika (KCU Ltd) hapo Jana (Julai 24,2013).
|
Rais Kikwete
akihutubia wananchi baada ya Kufungua jengo la kitega uchumi la Chama Kikuu cha
Ushirika (KCU Ltd).
|
Rais Kikwete akihutubia wananchi baada ya Kufungua jengo la kitega uchumi la Chama Kikuu cha Ushirika (KCU Ltd). |
Rais Kikwete
katika picha ya pamoja na viongozi wa KCU baada ya kufungua jengo la kitega
uchumi la Chama Kikuu cha Ushirika (KCU Ltd).
|
Rais
wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete amewasili
Mjini Bukoba tayari kushiriki katika
maadhimisho ya siku ya Mashujaa inayofanyika kitaifa Mkoani KAGERA leo(Julai
25,2013).
Mashujaa
wa Tanzania waliopigana Vita vya Kagera, wanakumbukwa leo(Julai 25,2013) katika
kilele cha sherehe hizo zitakazofanyika kwenye Kambi ya Kaboya mkoani Kagera.
Kwa
Mujibu wa Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Kanali Fabian Massawe amesema kuwa maandalizi yote yamekamilika na Rais
Jakaya Kikwete anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika shughuli hiyo
itakayoambatana na uwekaji wa mashada ya maua kuwakumbuka mashujaa hao.
Mashujaa
wa Tanzania wanakumbukwa leo baada ya kumpiga Fashisti Nduli Idd Amin, wakati
wa Vita vya Kagera vilivyopiganwa mwaka 1978 na 1979.
Katika
mapambano hayo, wapiganaji wa Tanzania wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa
Tanzania (JWTZ) waliyachakaza majeshi ya Nduli Amini wa Uganda.
Mbali
na hayo, Rais Kikwete anatarajiwa kuzindua Wilaya mpya ya Kyerwa iliyomegwa
kutoka Wilaya ya Karagwe,Kivuko cha Rusumo wilayani Ngara pamoja na kuzindua mradi wa kuzalisha umeme wa
Kaishozi.
Awali
maadhimisho ya Siku ya Kumbukumbu ya Mashujaa Tanzania yalikuwa yakifanyika
kila Septemba Mosi, lakini tarehe hiyo ilibadilishwa na kuwa Julai 25 kwa kuwa
ndiyo tarehe waliyopokewa mashujaa hao waliopigana vita vya Kagera.
Hii
ni mara ya pili kwa Mkoa wa Kagera kuandaa sherehe hizo ambapo Mara ya kwanza ilikuwa mwaka 2009.
Rais
wa Zanzibar, Ali Mohamed Shein na baadhi ya mawaziri akiwamo, Prof Anna
Tibaijuka (Nyumba na Maendeleo ya Makazi), Khamis Kagasheki (Maliasili na
Utalii), Harisson Mwakyembe (Uchukuzi), Hawa Ghasia (Tawala za Mikoa na
Serikali za Mitaa), Sospeter Muhongo (Nishati na Madini), John Maghufuli
(Ujenzi), Mathias Chikawe (Katiba na Sheria), Tersa Huvisa (Waziri wa Nchi
Ofisi ya Makamu wa Rais, Mazingira) ni miongoni mwa viongozi wanaoshiriki
sherehe hizo.
Baada
ya kuwasili katika Uwanja wa ndege wa Bukoba , Rais Kikwete ameweka jiwe la
Msingi la Mradi wa ukarabati na upanuzi wa uwanja wa ndege wa Bukoba.
Katika
hotuba yake fupi kabla ya kuweka jiwe la Msingi Rais Kikwete, Amesema ametimiza
ahadi yake kwa kukarabati ujenzi wa uwanja huo.
Awali
Waziri wa Uchukuzi Dk Harrison Mwakyembe amesema serikali itaendelea na kazi ya
kujenga viwanja vya ndege katika baadhi ya mikoa hapa nchini.
Mradi
wa ukarabati wa upanuzi wa uwanja wa ndege wa Bukoba umegharimu zaidi ya
shilingi Bilioni 21 kwa ufadhili wa
Benki ya Dunia na serikali ya Tanzania.
Mradi
huo ulioanza February 2012 unatarajiwa kumalizika February 2014.
No comments:
Post a Comment