|
Rais wa Tanzania Jakaya Kikwete akiwa
katika ziara yake ya Kikazi Mkoani Kagera leo (Julai 26,2013) amezindua barabara yenye kiwango cha Lami ya
Kagoma-Lusahunga wilayani Biharamulo mkoani Kagera yenye urefu wa kilometa 200
ambayo imekamilika kwa 97% ambapo sehemu iliyobaki ni mita 500 na
itakamili mwishoni mwa mwezi ujao.
|
|
Muonekano wa barabara yenye kiwango cha Lami ya
Kagoma-Lusahunga wilayani Biharamulo mkoani Kagera yenye urefu wa kilometa 200
ambayo imekamilika kwa 97% ambapo sehemu iliyobaki ni mita 500 na
itakamili mwishoni mwa mwezi ujao.
|
|
Rais wa Tanzania Jakaya Kikwete akiwasili
Wilayani Biharamulo mkoani Kagera kuendelea na ziara yake ya siku 6 mkoani humo
ambapo akiwa wilayani humo leo (Julai
26,2013) amezindua barabara yenye kiwango cha Lami ya
Kagoma-Lusahunga wilayani Biharamulo mkoani Kagera yenye urefu wa kilometa 200.
|
|
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr.Jakaya Kikwete akiwa jukwaa kuu pamoja na Waziri wa Ujenzi Dr.John Pombe Magufuri na Mkuu wa Mkoa wa Kagera Kanal mstaafu Fabian Masawe wakati walipo wasili Wilayani
Biharamulo mkoani Kagera kuendelea na ziara yake ya siku 6 mkoani humo ambapo
akiwa wilayani humo leo (Julai 26,2013)
amezindua barabara ya Lusahunga-Kagoma.
|
|
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr.Jakaya Kikwete mara baada ya uzinduzi wa barabara ,aliwahutubia
Wananchi na Kutoa wiki mbili kuanzia
sasa wanaomiliki silaha kinyume cha sharia kuzisalimisha haraka iwezekanavyo
sambamba na kuanza msako mkali kwa
majambazi yanayoteka magari na uvamizi mbalimbali katika Mikoa ya Kagera na
Kigoma kujisalimisha na kwamba baada ya
hapo Majeshi yote nchini yanaanza msako na wanawahusika hawatakamatwa mateka.
|
|
Katikati Ni Kamanda wa Polisi Mkoani Kagera Philip Kalangi akifuatilia hali ya Ulinzi na Usalama wakati
wa uzinduzi wa barabara ya
Lusahunga-Kagoma wilayani Biharamulo mkoani Kagera leo(Julai 26,2013).
|
|
Wananchi mbalimbali waliojitokeza kushuhudia uzinduzi wa barabara ya
Lusahunga-Kagoma wilayani Biharamulo mkoani Kagera leo(Julai 26,2013).
|
|
Waziri wa Ujenzi Dk John Pombe Magufuli akipinga ngoma ya Nyamigogo wakati
wa uzinduzi wa barabara ya
Lusahunga-Kagoma wilayani Biharamulo mkoani Kagera leo(Julai 26,2013).
|
|
Baada ya Uzinduzi wa Barabara hiyo, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Dr.Jakaya Kikwete amepanda mti katika eneo la uzinduzi huliofanyika eneo la Njia
panda wilayani biharamulo mkoani Kagera ikiwa ni ishara ya Serikali kuhamasisha
upandaji miti na utunzaji Mazingira hapa nchini.
|
|
Pia Mawaziri aliombatana nao Waziri wa TAMISEMI Bi.Hawa Ghasia nae alishiriki zoezi la upandaji mti katika eneo la uzinduzi huliofanyika eneo la Njia
panda wilayani biharamulo mkoani Kagera ikiwa ni ishara ya Serikali kuhamasisha
upandaji miti na utunzaji Mazingira hapa nchini.
|
|
Baada ya Uzinduzi wa Barabara hiyo, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr.Jakaya Kikwete amepanda mti katika eneo la uzinduzi huliofanyika eneo la Njia panda wilayani biharamulo mkoani Kagera ikiwa ni ishara ya Serikali kuhamasisha upandaji miti na utunzaji Mazingira hapa nchini. |
Rais Kikwete ambaye anaendelea na ziara yake ya siku
6 mkoani Kagera baada ya Kuzindua barabara ya Lusahunga –Kagoma wilayani
Biharamulo,Leo pia(Julai 26,2013) ameendelea na ziara yake wilayani Ngara ambapo amehutubia Wananchi wa Rulenge na Ngara
Mjini na kusisitiza Suala la Wahamiaji haramu kuondoka haraka nchini pamoja na na
Kutoa wiki mbili kuanzia sasa kwa wanaomiliki
silaha kinyume cha sharia kuzisalimisha haraka iwezekanavyo.
Pia Rais Kikwete amesema Serikali itaanza msako
mkali kwa majambazi yanayoteka magari na
kufanya uvamizi mbalimbali katika Mikoa ya Kagera na Kigoma ili kurejesha hali
ya usalama katika mikoa hiyo.
Aidha Raisi Kikwete katika ziara hiyo mkoani Kagera
ameambatana pia na Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo, Waziri wa Ujenzi Dr. John Pombe Magufuli, Waziri wa Maji Profesa Jumanne
Maghembe, Waziri wa Uchukuzi Dr. Harrison Mwakyembe , Profesa Anna Tibaijuka (Waziri
wa Nyumba na Maendeleo ya Makazi),Bi. Hawa Ghasia (Waziri Tawala za Mikoa na
Serikali za Mitaa-TAMISEMI).
Mawaziri hao kila mmoja kwa nafasi yake walilazimika
kujibu Hoja na Kero mbalimbali zilizokuwa zikitolewa na Wabunge kwa Niaba ya
Wananchi wao katika sekta ya Maji,Umeme,Barabara,Ardhi pamoja na Kero za
Uongozi katika Halmashauri ambapo wameahidi kuzifanyia kazi ili kusukuma mbele
maendeleo ya wananchi mkoani Kagera.
Aidha Rais Kikwete ataendelea na ziara yake
kesho(Julai 27,2013) kwa kuzindua Kivuko cha Rusumo wilayani Ngara ,kasha kuelekea
wilayani Karagwe na hatimae kumaliza ziara yake ya Kikazi mkoani Kagera .
No comments:
Post a Comment