Maadhimisho ya Mashujaa Kitaifa Mkoani Kagera yapendeza huku Rais Kikwete akiwaahidi kutatua Mgogoro wa Ardhi kati ya Wananchi na Kambi ya Kaboya Wilayani Muleba. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, July 25, 2013

Maadhimisho ya Mashujaa Kitaifa Mkoani Kagera yapendeza huku Rais Kikwete akiwaahidi kutatua Mgogoro wa Ardhi kati ya Wananchi na Kambi ya Kaboya Wilayani Muleba.


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiweka ngao/sime katika mnara wakati wa maadhimisho ya kumbukumbu ya Mashujaa Kitaifa Mkoani Kagera yaliyofanyika katika kambi ya jeshi ya Kaboya, Mjini Bukoba, mkoani Kagera leo Julai 25, 2013.





Viongozi wa dini wakisoma dua kwenye maadhimisho hayo. Pembeni ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Mohamed Ali Shein, Makamu wa Rais Dkt Mohamed Gharib Bilali, Jaji Mkuu Mheshimiwa Chande Othman na Jaji Mkuu wa Zanzibar Mhe Othman Makungu.




Rais Jakaya Kikwete akitembelea makaburi ya mashujaa waliopoteza maisha wakati wa vita na Nduli Iddi Amini wa Uganda.


Rais Jakaya Kikwete JK akisalimiana na askari wastaafu  wakati wa maadhimisho ya kumbukumbu ya Mashujaa Kitaifa Mkoani Kagera katika kambi ya jeshi ya Kaboya, mjini Bukoba, mkoani Kagera leo Julai 25, 2013.








Rais Kikwete Wananchi wakifuatilia hotuba fupi ya rais wa jamhuri ya muungano Tanzania baada ya kuweka dhana za asili kwenye mwenge wa kudumu katika  makaburi ya mashujaa na amesisitiza kuwa ulinzi na usalama umeimarika katika mkoa na nchi ya tanzania, kutokana na kauli ya mkuu wa majeshi Jenerali DAVIS MWAMUNYANGE, kuwahahikishia wananchi kuwa jeshi liko imara na linazingatia ulinzi kwa wananchi wake.


Wananchi wakifuatilia hotuba fupi ya rais wa jamhuri ya muungano Tanzania baada ya kuweka dhana za asili kwenye Mwenge wa Kudumu katika  makaburi ya mashujaa wakati wa maadhimisho ya kumbukumbu ya Mashujaa Kitaifa Mkoani Kagera yaliyofanyika katika kambi ya jeshi ya Kaboya, Bukoba, mkoani Kagera leo Julai 25, 2013.


Katika hatua nyingine, Rais Kikwete amewaahidi Wananchi wa Wilaya ya Muleba Mkoani Kagera kupima ardhi na Kuondoa Mgogoro kutokana na Kupakana na Kambi ya Kaboya. 




Hatua hiyo imekuja  baada ya mbunge wa jimbo la Muleba kaskazini CHARLES MWIJAGE, kumtajia rais mambo yanayowasumbua wananchi wa jimbo hilo,  alipotakiwa na rais kutaja matatizo yanayowakabili wananchi wilayani humo.




 Mheshimiwa Mwijage, amesema kuwa mgogoro wa wananchi na kambi ya Kaboya, aueleweki kutokana na kutokuwapo mipaka ya kambi hiyo, kitendo kinachosababisha wananchi washindwe kutumia ardhi kutokana na masuala ya ulinzi na usalama, ilhali jeshi nalo linatakiwa kuheshimia.




 Aidha  mbunge huyo amesema kuwa wananchi wakabiliwa na ukosefu wa huduma ya umeme, ambapo walishapewa ahadi ya kupatiwa huduma hiyo kupitia REA, lakini hadi sasa hakuna kilichoishatekelezwa na kusababisha lawama kwa viongozi wa jimbo hilo.




Rais Kikwete ameendelea na ziara yake mkoani Kagera, ambapo sasa yupo wilayani Muleba ambapo atahutubia wananchi baada ya kuzindua mradi wa maji katika eneo la IYAKO, na bada ya hapo anapumzika na kuelekea wilayani Biharamulo na Ngara mkoani Kagera ambako akiwa wilayani Ngara atazindua Kivuko cha Rusumo pamoja na kufanya mikutano ya hadhara na Wananchi wa Rulenge na Ngara mjini hapo kesho Ijumaa(Julai 26,2013).


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad