Kiemba aipa Simba ushindi wa bao 4-1 dhidi ya Maafande wa JKT Oljoro na kujiimarisha kileleni mwa Ligi kuu Vodacom Tanzania bara. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, October 07, 2012

Kiemba aipa Simba ushindi wa bao 4-1 dhidi ya Maafande wa JKT Oljoro na kujiimarisha kileleni mwa Ligi kuu Vodacom Tanzania bara.

Simba SC
Wekundu wa Msimbazi Simba SC imezidi kujiimarisha kileleni mwa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, kufuatia ushindi wa mabao 4-1 ilioupata  leo kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam dhidi ya timu ya JKT Oljoro ya Arusha  ambayo ilimaliza pungufu ya wachezaji wawili baada ya kipa wake Shaibu Issa na mshambuliaji Meshack Nyambele kutolewa kwa kadi nyekundu kipindi cha pili.


Katika mechi hiyo iliyochezeshwa na refa Amon Paul wa Mara, aliyesaidiwa na Anold Bugabo wa Singida na Charles Simon wa Dodoma, hadi mapumziko Simba walikuwa tayari mbele kwa mabao 2-1, mabao yake yote yakitiwa kimiani na kiungo Amri Ramadhan Kiemba katika dakika za 16 na 44, wakati la Oljoro lilifungwa na Paul Nonga dakika ya 29.


Kiemba alifunga bao la kwanza akiunganisha krosi pasi ya Christopher Edward, wakati bao la pili lilitokana na krosi ya Nassor Masoud ‘Chollo’, yote kutokana na mashambulizi ya upande wa kulia.


Nonga naye alifunga bao lake baada ya kupewa pasi ndefu na kumpiga chenga kipa na Nahodha wa Simba, Juma Kaseja upande wa kulia mwa Uwanja na kuutumbukiza mpira nyavuni kiulaini.


Kipindi cha pili katika Dakika ya 83 Mganda Emanuel Okwi aliifungia Simba bao la tatu na katika dakika ya tatu ya muda wa nyongeza baada ya kutimu dakika 90 za mchezo, Okwi akiwa anaelekea kufunga tena, alikwatuliwa na kipa wa Oljoro Shaibu Issa na refa akaamuru penalti sambamba na kumtoa nje kwa kadi nyekundu ya moja kwa moja mlinda mlango huyo. 


Awali ya hapo, Oljoro ilimpoteza mchezaji mwingine, Nyambele dakika ya 78, ambaye alionyeshwa njano ya pili kwa rafu aliyomchezea Jonas Mkude. Nahodha Kaseja alitaka kwenda kupiga, lakini akazuiwa na Felix Mumba Sunzu akaenda kufunga bao la nne kwa mkwaju wa penalti.


Kwa ushindi huo, Simba imefikisha pointi 16 baada ya kucheza mechi sita, hivyo kuendelea kuongoza Ligi Kuu, ikifuatiwa na Azam yenye pointi 13, ingawa imecheza mechi tano.
Matokeo na ratiba Jumapili Oktoba 7

Mgambo Shooting 1 v  0 Polisi Morogoro (Uwanja wa Mkwakwani,Tanga)
Toto Africans 2 v 1 JKT Ruvu (Uwanja wa Kirumba, Mwanza)
Tanzania Prisons 0 v 0 Mtibwa Sugar (Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine, Mbeya)

Jumatatu Oktoba 8

Kagera Sugar v Yanga (Uwanja wa Kaitaba, Bukoba)









































No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad