Bocco aing’arisha Simba SC na kujitanua Kileleni mwa VPL. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Tuesday, April 03, 2018

Bocco aing’arisha Simba SC na kujitanua Kileleni mwa VPL.

Wekundu wa Msimbazi Simba SC imejitanua kileleni mwa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara 2017/2018 baada ya ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya wenyeji, Njombe Mji FC jioni ya leo April 3,2018  kwenye uga wa Saba Saba mjini Njombe.

Pongezi kwa mfungaji wa mabao hayo yote mawili leo, Nahodha John Raphael Bocco ‘Adebayor’, moja kila kipindi na sasa Wekundi wa Msimbazi wanafikisha pointi 49 baada ya kucheza mechi 21, wakiwazidi kwa pointi tatu mabingwa watetezi, Yanga SC wenye pointi 46 za mechi 21 pia. 

Katika mchezo huo, Kiungo Haruna Niyonzima na beki Mbonde waliingia kipindi cha pili wakichukua nafasi za Emmanuel Okwi na James Kotei. 

Mbode na Niyonzima walikosekana dimbani kwa muda mrefu kutokana na kuwa majeruhi.

MSIMAMO WA LIGI ULIVYO SASA.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad