![]() |
|
Muonekano wa mashimo mawili barabarani katika barabara
ya Igunga –Singida linalotajwa kuwa chanzo cha ajali ya Basi la City Boy
kugongana uso kwa uso na Fuso eneo la Makomero ambapo tairi la Fuso lilipasuka
na kupoteza
muelekeo.
TAARIFA
RASMI NI HII TULIOIPATA KUTOKA KWA INSPECTOR HARDSON KAIMU RTO MKOA WA TABORA.
Gari T486
ARB FUSO ikiwa na mzigo wa viazi ikitokea singida kuelekea Igunga tairi ya
kulia litumbukia KTK mashimo mawili barabarani kisha kupasua tairi na rim
kupinda & mfumo wa usukani kukatika maungio ya steering rod na steering box
kisha gari kukosa uelekeo na kugonga basi la abiria T983 DCE Scania kampuni ya
city boy.
Jumla ya watu 12 wamepoteza maisha , 10 eneo la tukio, 2 wakiwa
wanapelekwa Hospitali ya Wilaya ya Igunga.
Jumla ya
majeruhi 46 wamefikishwa Hospitali ya wilaya ya Igunga kwa matibabu, kati yao 3 ni mahututi
amapo ME 02 wamepelekwa Hospitali ya Rufaa ya Bugando Mwanza na KE 01 amepelekwa Hospitali ya Nkinga .
Dereva wa
basi amekufa papo hapo. Wahusika wa FUSO kwa taarifa za awali inasemekana
wamekimbia baada ya ajali hii.
|
![]() |
|
Waziri wa
Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba ameliagiza Jeshi la Polisi
kuwatoza faini, kuwaweka ndani madereva wanaovunja sheria za barabarani na
kusababisha ajali kizembe na wasiachiwe mpaka watakapofikishwa Mahakamani.
Mwigulu
ametoa agizo hilo Alhamisi, Aprili 5, 2018 bungeni Mjini Dodoma wakati
akitoa taarifa ya ajali iliyotokea wilayani Igunga usiku wa kuamkia leo, ajali
iliyohusisha lori aina ya fuso na basi la abiria la Kampuni ya City Boys na
kuua watu 12 huku wengine 46 wakijeruhiwa.
“Taarifa za
awali tulizopewa zilieleza chanzo cha ya ajali hiyo sio mashimo ya barabarani
pekee yake bali ni mwendokasi wa dereva wa fuso ambaye aliligonga basi hilo.
Wengine walipita mchana kutwa kwenye hayo mashimo yeye akaja kusababisha ajali
usiku.
Naliagiza Jeshi la Polisi popote pale watakapomkamata dereva anatembea
mwendokasi pamoja na hiyo ya kutoza faini, wamuweke ndani wasimuachie mpaka
pale watakapompeleka Mahakamani ili hatua zaidi ziweze kuchukuliwa”, amesema
Mwigulu.
Pamoja na
hayo, Mwigulu ameendelea kwa kusema “endapo dereva huyo akitoka Mahakamani na
kama rekodi zake ni mwendokasi basi anyang’anywe leseni yake ili asiweze
kuendelea kuendesha magari yanayosababisha ajali na kupoteza maisha ya watu
kama hivi jana ilivyotokea”.
Aidha, Rais
Magufuli amewataka viongozi wote wanaohusika na usimamizi wa usalama wa
barabarani kutafakari kwa nini ajali nyingi zimekuwa zikitokea katika maeneo
yaleyale na kutafuta ufumbuzi ili kuepusha madhara ya watu kupoteza maisha,
kupata ulemavu wa kudumu na kupoteza mali.
|
![]() |
|
Aidha Ujumbe wa Umoja Wa Madereva Wa Mabasi Makubwa Tanzania - Uwamata
wameomba ;….Nadhani
ifike kipindi sasa kila MTU awajibike kwa nafasi yake, ndugu zetu TANROAD mkoa
wa TABORA haya mashimo tunayapigia sana kelele ,sitaki kuamini kwamba hayaoni na
msisubiri mpaka yatokee maafa ndo mtengeneze hayo mashimo kama ilivyokua
changarawe pale mafinga nayo ilikua kama hii.
Eneo
hatarishi kwa mashimo ni Nyasamba, Hungumalwa, Mwanza, Nanga, Igunga road, Makomero,
n.k tunawaombeni sana mzibe haya mashimo.
Fuatia tamko
lako lile tu la Bungeni tayari madereva wengi usiku huu wanalala lockap kisa
wemezidisha speed 82 badala ya 80 achilia mbali tumepewa ziada ya ya speed 5 na
gari zina VTS.
|








No comments:
Post a Comment