Bakoba FC na Hazina ya Ubingwa wa Makombe ma3 Manispaa ya Bukoba. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Tuesday, April 03, 2018

Bakoba FC na Hazina ya Ubingwa wa Makombe ma3 Manispaa ya Bukoba.

Nahodha wa timu ya Bakoba Fc akiwa amebeba Kombe la Ubingwa leo hii jioni kwenye Uwanja wa Kaitaba mara baada ya kuibuka Kidedea kwa kuifunga Timu ya Ijuganyondo bao 3-0. Katika Mchezo huo Kipindi cha kwanza hakuna Timu iliyopata bao kipindi cha kwanza, Kipindi cha pili goli zote tatu zilipatikana Goli la kwanza likifungwa na Denis Msuva, Bao la pili lilifungwa na Datius Peter na bao la tatu lilifungwa na Ezekiel Izack aliyekuwa amevaa jezi namba 10. Bingwa huyo ameondoka pia na fedha Tsh Milioni 2.5 .
 Bakoba FC anafanikiwa sasa kujikusanyia makombe matutu ya Kagasheki Cup,Kamanda wa Polisi Kagera-Ollomi Cup na Kamala Cup.
  Picha zote na Faustine Ruta, Bukoba.
Picha ya pamoja ya Mabingwa Bakoba FC na Mdhamini wa Ligi hiyo ya Kamala Cup 2018 pamoja na Mgeni rasmi na Viongozi wengine.
Mabingwa Bakoba FC wakiwa wamebeba Mwali wao.

Ligi hii ya Kamala Cup 2018 ilianza Mwezi Februari tarehe 18, 2018 na kushirikisha Timu za Kata 16 na hii leo April 2, 2018 imehitimishwa kwa Timu ya Bakoba kuibuka Bingwa.

Mshindi wa Pili wa mashindano hayo , Ijuganyundo FC aliondoka na Tsh Milioni 1.8 huku wa 3 Timu ya Kitendaguro FC ikiondoka na Tsh Milioni 1.2.
Ndg. Salum Umande Chama akiongozana na  Mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya Bukoba Bw. Deodatus Kinawilo pamoja na mdhamini wa Ligi hii Diwani Kamala Kalumuna (kulia) kwenda Uwanjani kukabidhi Wachezaji zawadi zao.
Mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya Bukoba Bw. Deodatus Kinawilo akitoa neno wakati wa ufungaji wa Ligi hiyo ya Kamala Cup 2018. 

Mkuu wa Wilaya Bukoba  Deodatus Kinawilo (katikati) ndiye alikuwa mgeni Rasmi katika Fainali hii iliyohitimishwa April 2, 2018 na kukitaka Chama cha Soka mkoa KRFA kwa kushirikiana na Vyama vya Soka ngazi za wilaya kuhakikisha kupitia mashindano madogo madogo yanayochezwa mkoani humo ili kuibua Timu nyingine zitakazoungana na Timu ya Kagera Sugar Ligi kuu. 

Naye muandaaji wa Mashindano hayo ya Kamala Cup 2018 , Diwani Kamala Kalumuna amebainisha kuwa Jumala ya Tsh Milioni  11.8 kukamilika na  Timu ya Bakoba Kuibuka Kidedea kwa kuifunga Timu ya Ijuganyondo Fc Bao 3-0.  

Picha zote na Faustine Ruta, Bukoba.
Kikosi cha Timu ya Bakoba FC kilichoifumua Ijuganyondo Fc kwenye mchezo wa fainali Kamala Cup 2018.
Kikosi cha Timu ya Ijuganyondo Fc kilichoanza mchezo wa fainali Kamala Cup 2018.
Wachezaji wa Timu ya Ijuganyondo wakiomba katikati ya Uwanja muda mfupi na kuanza mchezo huo kwa kasi ambao mpaka kipindi cha kwanza kinamalizika ilikuwa 0-0.




Mkuu wa Wilaya Bukoba Bw. Deodatus Kinawilo(katikati) kulia ni Ndg. Salum Umande Chama wakiwa meza kuu.

Ndg. Salum Umande Chama akiteta jambo na Mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya Bukoba Bw. Deodatus Kinawilo meza kuu wakati mtanange unaendelea.
Mwali wa mshindi wa Kwanza Kamala Cup 2018.
Makombe ya Mshindi wa Kwanza, wa Pili na Watatu Kamala Cup 2018.

Huku Mashabiki wakimpogeza kwa Ligi hiyo ambayo ilikuwa ikishehenesha Mashabiki kibao Uwanjani hapo Kaitaba. Pia Mdhamini huyo amesema Ligi hiyo ni Endelevu na Mwaka kesho 2019 ataiboresha zaidi ya mwaka huu.

Taswira mbalimbali uwanjani Kaitaba ,watu waliingia kwa wingi wakati wa Fainali Kati ya Timu ya Bakoba FC dhidi ya Ijuganyondo FC.
Kipa wa Ijuganyondo Fc hakuona ndani....
2-0 Baadhi ya Wachezaji wa Bakoba Fc wakipongezana kwa bao.


3-0 Ezekiel Izack akipongezwa kwa kumwagiwa maji mara baada ya kuipachikia bao la tatu Timu ya Bakoba FC.






Mashabiki mnasemaje?????

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad