Vichwa hivyo 11 viliingizwa nchini katika
bandari ya Dar es Salaam Julai 2017 na kampuni ya Progress Rail Locomotives ya
Marekani, PRL, kwa ajili ya kuviuza.
Shirika la Reli nchini, TRC leo limenunua
vichwa kumi na moja vya treni kwa bei ya dola Milioni Nane na Laki Nane ili kuliongezea
ufanisi wa kazi shirika hilo.
Taarifa ya Mkurugenzi Mkuu was TRC, Msanja
Kadogosa imesema kwa sasa TRC ina vichwa 29 madhubuti kati ya 47
vinavyovihitajika ili kutoa huduma bora zaidi.
Vichwa hivyo 11 viliingizwa nchini katika
bandari ya Dar es Salaam Julai 2017 na kampuni ya Progress Rail Locomotives ya
Marekani, PRL, kwa ajili ya kuviuza.
Kwa kuhitaji vichwa hivyo serikali iliunda
timu ya wataalam kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, TEMESA na TRC kwa ajili
ya kubaini kama vichwa hivyo ni vipya au la.
Baada ya uchunguzi na ukaguzi wa vichwa hivyo,
kamati ilibaini kuwa ni vipya na hivyo serikali kuamua kutiliana saini na
kampuni ya PRL ili kuvinunua.
Hata hivyo ili kujihakikishia zaidi ubora
wake, vichwa hivyo vitafanyiwa majaribio katika awamu tatu, ikiwemo kuvitazama
kwa nje, kuviwasha na kuvipa mzigo vikiwa havitembei na tatu ni kuvifunga
kuvuta mabewa vikiwa na mzigo wa tani 700 kutoka Dar es Salaam hadi Morogoro na
kuviongezea mzigo wa tani 1,200 kutoka Morogoro hadi Kigoma na Mwanza.
TRC imetiliana saini leo March 16,2018 jijini Dar es Salaam
na kuvinunua vichwa hivyo, huku TRC ikihakikishiwa ubora wa vichwa hivyo kwa
garanti ya miaka miwili.
|
Friday, March 16, 2018
Serikali yavinunua Vichwa vya Treni vilivyokwama Bandarini.
Tags
# HABARI
Sambaza Hii
Chief Editor | Mhariri
HABARI
Labels:
HABARI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Kuhusu Mwandishi
Journalist / Chief Editor / Tanzanian Blogger
Simu: 0756830214 / 0620197747 / 0789925630.
No comments:
Post a Comment