Basi la Kampuni ya KIMOTCO (pichani)
lililokuwa likitoka Musoma,kwenda Arusha kupitia Mugumu,limepinduka katika mto
unaodaiwa kuwa na viboko ndani ya hifadhi ya Taifa ya Serengeti.
Mhifadhi Mkuu wa hifadhi hiyo William Mwakilema amethibitisha kupata taarifa ya tukio hilo leo Machi 16,2018 na kusema kuwa katika ajali hiyo hakuna majeruhi wala vifo,na kuwa abiria wote walitoka ndani ya basi hilo na kukaa juu ya basi kusubiri msaada wa kuokolewa. Jitihada za kuwaokoa mmoja mmoja zilifanyika.
Baada ya basi hilo kusombwa na maji abiria
wote walitokea juu ya madilisha ya basi na kukaa juu yake,kwani halikuzama
lote,jitihada za kuwaokoa zinaendelea mpaka sasa,ambapo zaidi ya abiria
wanne wametolewa.
TAARIFA ZAIDI TUNASUBIRI KUTOKA MAMLAKA HUSIKA |
Baadhi ya Abiria wakiwa juu ya basi hilo
mara baada kupinduka,wakiokolewa mmoja mmoja na Lori kama ionekanavyo.
|
No comments:
Post a Comment