Kupitia kwa
mpango huo kabambe, kila nchi itapata nyongeza ya megawati 26.6 katika gridi
zao za taifa na hili linatarajiwa pia kuimarisha uunganishwaji umeme wa kikanda
baina ya nchi hizo tatu ambazo pia ni wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki
(EAC).
|
“Kukamilika
kwa mradi huu kutanufaisha kaya elfu saba (7,000) kupitia mpango wa maendeleo
katika serikali za mitaa na kaya nyingine 188 zinazozunguka mradi huu,” ilisema
taarifa hiyo na kuongeza kuwa inategemewa pia wakati wa utekelezaji wa mradi
huu kabambe wa kikanda katika eneo la Afrika Mashariki, kutakuwa na ajira kwa
zaidi ya wafanyakazi 500 wenye weledi, weledi wa kati na vibarua kutoka nchi
tatu zitakazonufaika na mradi huu.
Ujenzi wa
mradi unatarajiwa kutekelezwa kwa miaka mitatu na utakamilika mwaka 2020.
Makandarasi wawili kutoka China, CGCOC Group Ltd na Jiangxi Water &
Hydropower Construction Company Ltd (CGCOC - JWHC JV) watajenga bwawa la maji
pamoja na miundombinu mingine.
|
Kwa upande
mwingine, muunganiko wa makandarasi wawili Rusumo Falls Andritz Hydro GmbH ya
Ujerumani na Andritz Hydro PVT Ltd ya India watahusika na ufungaji wa mitambo
ya kuzalisha na kusambaza umeme.
Mradi wa
kuzalisha umeme wa maji wa Rusumo unasimamiwa na taasisi ya Nile Equatorial
Lakes Subsidiary Action Program Co-ordination Unit (NELSAP-CU) iliyopewa jukumu
hilo na nchi tatu wanufaika kupitia Kampuni ya Rusumo Power Ltd (RPCL),
inayomilikiwa kwa pamoja na mashirika ya umeme katika nchi za Tanzania, Rwanda
na Burundi.
|
No comments:
Post a Comment