Meja
Jenerali Michael Isamuhyo akipenya kwenye vichaka wakati wa kukagua eneo
litakalojengwa ukuta.
Jeshi
la Ulinzi la Wananchi Tanzania JWTZ limeanza kutekeleza agizo la Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli aliyelitaka
kujenga uzio wa kuzunguka kitalu A hadi D katika eneo madini ya tanzanite,
Mirerani Wilaya ya Simanjiro mkoani Manyara ili kudhibiti uchimbaji na biashara
ya madini hayo.
Dk Magufuli September 20,2017 aliiagiza JWTZ kwa kushirikiana na Shirika la Uchumi la Jeshi la Kujenga
Taifa (Suma JKT) kuanza mara moja kujenga uzio kwenye eneo la kitalu A hadi D
lililopo eneo la Simanjiro ambalo kunapatikana madini ya kipekee ya tanzanite.
Aidha, aliagiza kufungwa kwa kamera maalumu, kuweka fensi maalumu na kutakuwa
na eneo moja la mlango wa kutokea na kuingia ili kubaini wezi wanaoiba madini
hayo.
|
Jana September
21,2017, Meja Jenerali Michael Isamuyo akiwa na wataalamu wa JWTZ, wamefika
Mirerani kwa helikopta na kisha kukagua eneo lenye vitalu vya tanzanite wakiwa
angani na baadaye wakatua na kukagua wakiwa ardhini kwa kutumia magari na
kutembea kwa miguu.
Akizungumza baada ya kutua kwenye uwanja wa wazi wa
Mererani, Meja Jenerali Isamuyo alisema JWTZ imeanza kutekeleza agizo la Rais
na Amiri Jeshi Mkuu mara moja na ipo tayari kukamilisha kazi kama
ilivyokusudiwa.
|
Meja
Jenerali Isamuyo alisema baada ya kutembea kwa miguu katika eneo la vitalu A
hadi D, amebaini kuwa eneo linalopaswa kujengwa uzio huo ni la kawaida na
ametaka wananchi watoe ushirikiano wa kutosha wakati wa ujenzi wa uzio huo.
Alionya kuwa wakati wa utekelezaji wa jukumu
hilo, JWTZ haitarajii kukwamishwa na mtu yeyote na haitakuwa tayari kukwamishwa
kwa namna yoyote.
Baadhi ya
viongozi wa Chama cha Wachimbaji wa Madini wa Mkoa wa Manyara waliokuwepo
wakati Meja Jenerali Isamuyo akitua na akikagua eneo la vitalu vya tanzanite,
walimpongeza Rais Magufuli kwa kuagiza kujengwa kwa uzio huo na wameahidi kutoa
ushirikiano wa kutosha wakati wa ujenzi huo.
|
Meja
Jenerali Michael Isamuhyo akioneshwa ramani ya vitalu A hadi D katika eneo la
madini ya Tanzanite huko Mererani.
|
Meja
Jenerali Michael Isamuhyo akisalimiana na baadhi ya wakazi wa eneo la
Mererani,mara baada ya kutua katika uwanja wa wazi wa Mererani, Wilaya ya
Simanjiro Mkoani Manyara
|
Helkopta
iliyombeba Meja Jenerali Michael Isamuhyo ikitua katika uwanja wa wazi wa Mererani,
Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara tayari kwa kukagua eneo litakalojengwa uzio
kuzunguka kitalu A hadi D katika eneo la Madini la Tanzanite Mererani ikiwa ni
utekelezaji wa agizo la Rais Dkt. John Pombe Magufuli
|
No comments:
Post a Comment