Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli leo Aprili 28, 2017
amepokea rasmi taarifa ya Uhakiki wa Watumishi wa Umma nchini wakati wa hafla
ya maadhimisho ya miaka 10 ya Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).
Akikabidhi
taarifa hiyo kwa Rais Magufuli, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais- Utumishi na
Utawala Bora, Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki, Rais amesema kuwa, Wizara yake
iliagiza NECTA kuhakiki vyeti vya kidato cha nne, cha sita na vya uwalimu.
“Jumla ya
watumishi wa umma 435,000 wamefanyiwa uhakiki wa vyeti vyao vya taaluma,
Watumishi 9932 kati ya watumishi waliohakikiwa walikutwa na vyeti vya kughushi,
Vyeti vyenye utata. Vyeti 1538 vilikuwa vikitumiwa na jumla ya watu 3076”
Akihutubia
baada ya kupokea taarifa hiyo, Rais Magufuli amewataka watumishi 9,932
waliobanika kuwa na vyeti vya kugushi waondoke kazini mara moja, na kuagiza
mamlaka zilizowaajiri kukata mishahara yao huku akiongeza kuwa kwa wale
watakaobakia kazini hadi Mei 15, wakamatwe ili sheria ichukue mkondo wake
ikiwemo kufungwa jela miaka 7.
“Mtu
aliyeghushi vyeti hatuwezi kumsamehe, wote ataondoka mara moja, mishahara yao
ikatwe kabisa”
“Hao
watumishi 9,932 wenye vyeti feki wenyewe kazini mara moja, watumishi wenye
vyeti feki ambao watakaidi na kubaki kwenye ajira hadi Mei 15, wakamatwe
wafikishwe kwenye vyombo vya sheria wafungwe hiyo miaka 7.
“Wanaotumia cheti kimoja watu wawili,
wasiwekewe mshahara ya mwezi huu, na kama wanajijua wajisalimishe, pia nikuombe
Waziri utangaze mara moja nafasi za kazi 9,932 za watumishi wenye vyeti feki
ambao wametakiwa kuondoka mara moja kazini ili zichukuliwe na watu wengine
wenye vigezo.” Alisema Rais Magufuli.
MSIKILIZE RAIS MAGUFULIA AKITUMBUA JIPU
|
No comments:
Post a Comment