Zifuatazo ni
njia zakufanya ukisha nunua simu yenye betri mpya ama betri mpya.
A) Hakikisha
unaiwasha kwanza simu hiyo na kujua ina aslimia ngapi. Kama utaiwasha na
kuikuta ina chaji asilimia 49% na kushuka chini, unashauriwa uizime na uichaji
simu hiyo kwa muda wa masaa matatu. Kwa kuchaji muda huo, itasaidia betri kujaa
vizuri zaidi.
B) Endapo
umewasha na ukakuta betri asilimia 50% na kuendelea juu, unashauriwa kuitumia
simu hiyo mpaka chaji ifike asilimia 10% na kisha uichaji kwa masaa matatu ili
iweze kujaa vizuri zaidi.
C) Kila
ifikapo asilimia 10% ya chaji ni muhimu kukumbuka kuichaji simu yako,
unashauriwa kuichaji simu yako hiyo ikiwa imezimwa kwa masaa mawili. Kwa
kuzingatia hayo Betri ya simu yako itadumu kwa muda mrefu.
|
Epuka
kuchaji simu yako mara kwa mara kwa kuhofia chaji kwani kufanya hivyo humaliza
nguvu ya betri yako kwenye simu. Pia usiweke simu yako karibu na vitu
vinavyoweza kuua nguvu ya betri.
|
No comments:
Post a Comment