Mkurugenzi Mkuu wa TCRA Mhandisi
James Kilaba.
Mamlaka ya
Mawasiliano Tanzania (TCRA) imetoka tahadhari kwa watumiaji wa simu za mkononi
kutorudisha pesa kwa mtu aliyekutumia pesa kimakosa.
Tahadhari
hiyo ilitolewa Jana April 27,2017 na Mtakwimu kutoka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA),
Batholomew Marcel wakati akiwasilisha mada iliyohusu Ukuaji wa Sekta ya
Mawasiliano na Tahadhari za Kuzingatiwa na Mtumiaji wa Huduma na Bidhaa za
Mawasiliano katika warsha kuhusu Mradi wa Kukuza Utawala Bora na Uwajibikaji
Tanzania kupitia teknolojia ya dijitali, iliyofanyika Dar es Salaam.
“KAMA kuna
pesa imetumwa kimakosa kwenye simu yako, hata kama mwenye simu aliyekutumia
kimakosa atakuomba na kukubembeleza, usimrudishie yeye, bali ziache na
uijulishe kampuni ya simu inayohusika wao ndio wamrudishie” alisema Batholomew.
Aliwatahadharisha
Watanzania kuwa makini kwani hali hiyo inaweza kuwasababishia hasara na pengine
kuwaingiza katika mikono ya sheria za nchi kama tuhuma za uhalifu mwingine
wowote, licha ya nia nzuri inayoweza kuwapo kwa mrudisha pesa.
Alisema
inayepokea pesa iliyotumwa kwake kimakosa anapaswa kuijulisha kampuni husika ya
simu vinginevyo anaweza kujikuta anafanya malipo na kutuma pesa kwa wahalifu
huku mifumo ikionesha pesa ilikwenda kwake.
Alisema
kutokana na kukua kwa teknolojia ya habari na mawasiliano (ICT), watu wengi
wanatumia simu kutunza, kupokea na kutuma pesa zao hivyo, mikakati bora zaidi
haina budi kuwapo ili kuepusha uhalifu wa kimtandao hususani kuhusu pesa
mtandao.
“Hapa lazima
kuwa makini kwani teknolojia hii ya pesa mtandao pia ina changamoto nyingi na
hatari. Kazi ya kurudisha pesa kwa aliyetuma kimakosa, iache ifanywe na kampuni
husika ya simu yaani mtoa huduma sio wewe,” alisema.
Changamoto
nyingine Marcel alisema ni pamoja na kuibuka wimbi la matapeli wanaojifanya
kumfahamu mtu huku wenyewe wakijifanya ni wanasiasa, viongozi wa kikazi,
kiserikali, kidini au wanafamilia wanaotoa maelekezo ya kumtaka mtu afanye
malipo, kutuma pesa au kuhitaji msaada kwa ulaghai.
Aliwataka
watumiaji wa huduma hizo kuwa makini kwani makosa ya kimtandao ni makosa kama
yalivyo mengine na yana sheria zake ikiwamo Sheria ya Makosa ya Mtandao ya
Mwaka 2015.
Akasema,
“Epuka kutunza pesa nyingi katika chombo kimoja kama simu, ukipoteza simu toa
kwanza taarifa kwa kampuni husika ya simu ili waifunge kisha sasa, toa taarifa
polisi na pia, badili password (namba ya siri) mara kwa mara walau kila baada
ya siku 90.”
Akaongeza,
“Wengine wanaokumbwa au kulizwa na changamoto za pesa mtandao, ni wale
wanaokubali kuaminishwa kuhusu kuwapo biashara inayozaa faida kubwa kwa muda
mfupi, kushinda bahati nasibu hata ambazo hawakushiriki na kupata mikopo
kirahisi, lakini wakatakiwa kutanguliza malipo,” alisema.
Akasisitiza,
“Kuwa makini kwa kuepuka mikopo au dili zinazokutaka kutanguliza fedha…” Kwa
upande mwingine, alisema zipo fursa nyingi za mitandao ikiwamo kufanya malipo
mbalimbalimbali yakiwamo ya huduma za kijamii kama maji, umeme na ankara
nyingine; pamoja na biashara huku wengine wakijiajiri au kuajiriwa katika sekta
hiyo ya pesa mtandao.
Katika hatua
nyingine, Afisa wa Programu wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHCR),
Pasience Mlowe, katika warsha hiyo aliiomba Serikali na watunga sera na sheria
kuzitazama upya sheria alizosema ni kandamizi ikiwamo Sheria ya Makosa ya
Kimtandao ya Mwaka 2015.
Katika
taarifa kuhusu namna Oxfam inavyotumia ICT duniani, Bill Marwa alisema ni
pamoja na kuwatumia watu wanaowasaidia na kukusanya pesa toka kwa wafadhili
mbalimbali. “Teknolojia hii inatusaidia kuokoa muda na pesa,” alisema.
|
No comments:
Post a Comment