Waziri wa
Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe,Hapo jana March 24,2017, baada ya
kuapishwa Ikulu jijini Dar es salaam, amekiri kuwa anafahamu kuhusu tukio la
uvamizi lililofanyika katika ofisi za Clouds Media Group.
Akizungumza
na waandishi wa habari, Waziri Mwakyembe aliyechukua nafasi ya aliyekuwa Waziri
wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Moses Nnauye alisema kuwa yeye kwa
sasa hawezi kulizungumzia tukio hilo wala kutoa uamuzi wowote kwa kuwa hajapata
ushahidi unaojitegemea.
“Ninachokijua
kuhusu hilo tukio kinatokana na taarifa za vyombo vya habari, taarifa za
magazeti, za redio, za televisheni, na sidhani kama taarifa hizo zinatosha kwa
mimi kutoa uamuzi wowote.”
Ameongeza
kuwa bado suala hilo ni la kuchunguzwa zaidi kwani picha inayotolewa ni ya
upande mmoja.
“Mlalamikaji
hapa ni Clouds, anayetupa taarifa kuhusu suala hili zima ni Clouds na wenzake.
Kwa hivyo naipata picha hii kwa upande mmoja…”
Aidha kwa
mujibu wa ripoti iliyokuwa imetolewa na kamati iliyoundwa na aliyekuwa Waziri,
Nape Nnauye ilisema kuwa wamesikiliza upande wa mlalamikaji (Clouds Media
Group).
Lakini
walipokwenda kwa ajili ya kuusikiliza upande wa mlalamikiwa (RC Paul Makonda)
hawakufanikiwa kumpata.
Hii ni baada
ya wao kusubirishwa kwa muda mrefu nje
ya ofisi yake na baadae kuambiwa kuwa Makonda ameondoka na hatoweza kurudi kwa
siku hiyo.
Jambo hili liliwafanya wajumbe hao kujiaminisha kuwa Makonda hakuwa
tayari kulizungumzia suala hilo na aliamua kuwatoroka.
Hata hivyo
ripoti hiyo ilikabidhiwa kwa aliyekuwa Waziri, Nape Nnauye ili aifikishe katika
mamlaka husika kwa ajili ya kuchukuliwa hatua zaidi.
|
No comments:
Post a Comment