Hii ilikuwa
ni Mechi ya Kwanza kwa Kocha Mpya wa Taifa Stars, Salum Mayanga na Nahodha Samatta kuipa bao Taifa Stars la kwanza dakika
ya 3 tu ya mchezo huo huku bao la pili
likifungwa dakika ya 87 kwa Frikiki murua ya Samatta.
|
Licha ya
kufunga magoli mawili, Samatta aliwa kwenye wakati mgumu kwa sababu mara nyingi
alikuwa akichezewa rafu zilizosababisha wachezaji wa Botswana kuoneshwa kadi za
njano. Samatta ilibidi atibiwe na daktari wa Stars baada ya kufanyiwa rafu
wakati akijaribu kumtoka moja ya mabeki wa Botswana.
|
Botswana,
chini ya Kocha Peter Buffler,
ilionyesha Soka la kuridhisha lakini ukali wa Mchezaji wa Kulipwa Samatta, anaechezea Timu ya KRC Genk
huko Belgium, ndio uliwaua.
Taifa Stars
inatarajiwa kucheza mchezo mwingine dhidi ya Burundi Jumanne ijayo, Machi 28,2017.
|
No comments:
Post a Comment