Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli Jana, July 30 2016
ameendelea na ziara yake katika Mkoa wa Tabora akitokea Mkoa wa Singida.
Mkoani
Tabora, Rais Magufuli amezungumza na wananchi waliosimamisha msafara wake katika
vijiji vya Nanga na Ziba na amefanya mikutano ya hadhara Igunga na Nzega ambako
amewahakikishia wananchi kuwa serikali yake itahakikisha inatekeleza ahadi
zilizopo katika Ilani ya Uchaguzi Mkuu ya Mwaka 2015.
Katika
mkutano wa hadhara uliofanyika Igunga, Rais Magufuli amepokea malalamiko ya
wananchi kuhusu kutoanza kutumika kwa kituo cha mabasi na soko na amewaagiza
viongozi wa Mkoa wa Tabora kuhakikisha kituo cha mabasi cha Igunga na soko la
Igunga vinaanza kutumika kuanzia Jumatatu ijayo ya tarehe 01 Agosti, 2016.
Kuhusu kero
ya maji, Dkt. Magufuli amesema Tanzania imepata mkopo wa dola za kimarekani
Milioni 268.35 kutoka nchini India ambazo zitatumika kutekeleza mradi wa
kusambaza maji ya ziwa Viktoria katika Miji ya Tabora, Igunga, Nzega, Sikonge
|
No comments:
Post a Comment