July 28, 2016 Chama cha mapinduzi
(CCM) kikiongozwa na msemaji wake Christopher Ole Sendeka kimekutana na waandishi wa habari Dar es
salaam na kuzungumzia hatua iliyotangazwa na chama cha demokrasia na maendeleo
CHADEMA kufanya maandamano ya nchi nzima.
"Jana tarehe 27/7/2016 chama cha
demokrasia na maendeleo (CHADEMA), walitoa kauli iliyojaa uongo mwingi za
kibabaishaji na kuthibitisha ukweli kuwa kwa hakika kutokana na kasi ya
serikali ya awamu ya tano chini ya Rais John Magufuli wapinzani wamekosa
ajenda.
"Katika uongo na uzushi
walioutangaza, CHADEMA wanasema wameamua kufanya mikutano na maandamano nchi
nzima, kimsingi hoja walizozitumia zimejaa upotoshaji na uongo uliokithiri.
Ifahamike kuwa serikali haijazuia mikutano kwenye majimbo yao.
"Wabunge wako huru kufanya
shughuli zao na tumeona baadhi ya wabunge wakifanya shughuli zao majimboni bila
shida wakiwemo hao wa upinzani.
"Ni vizuri tukakumbuka matukio
kwenye operesheni kama hizi yaliyopoteza maisha ya vijana wetu na matokeo ya kila
operation" –Ole Sendeka.
|
No comments:
Post a Comment