Wana lambalamba Azam FC walishindwa kulinda uongozi wa bao 2-0 na kutoka Sare 2-2
na JKT Ruvu katika Mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara iliyochezwa
huko Azam Complex, Chamazi, kwenye Viunga vya Jiji la Dar es Salaam .
Bao za Azam FC zilipatikana dakika za 31 na 37 kupitia kwa Bolou
na Kipre Tchetche na JKT Ruvu
kusawazisha Kipindi cha Pili Dakika za 56, kwa Penati ya Saadi Kipanga, na Bao jingine ni la Dakika ya 71 la Najim Magulu.
Huku kila Timu ikiwa imebakiza Mechi
3, Yanga SC wanaongoza Ligi kuu
wakiwa na Pointi 68 wakifuata Azam FC
wenye Pointi 60 na Simba SC ya 3
ikiwa na Pointi 58 wakiwa na Mechi 4 mkononi.
Hali hii inaifanya Yanga SC kuhitaji Pointi 3 tu katika
Mechi zao 3 zilizobaki ili watwae tena Ubingwa bila kujali matokeo ya Azam FC na Simba SC.
Lakini pia upo uwezekano wa Yanga SC kutwaa bila ya hata kutwaa
hizo Pointi 3 kwa vile Azam FC na Simba SC zina Mechi zao Mei 8 na Yanga SC Mechi yao inayofuata ni Mei 10
na ikiwa Azam FC na Simba SC zitateleza kwenye Mechi zao za
Siku hiyo basi Yanga SC atangazwa
Bingwa Siku hiyo hiyo.
LIGI KUU VODACOM 2015/2016 - RATIBA
Jumamosi Mei 7,2016.
JKT Ruvu v Ndanda FC
Stand United v Coastal Union
Mgambo JKT v Mtibwa Sugar
Jumapili Mei 8,2016.
Tanzania Prisons v Majimaji
Simba v Mwadui FC
Kagera Sugar v Azam FC
Jumanne Mei 10,2016.
Mbeya City v Yanga SC
Jumatano Me 11,2016.
Majimaji v Simba SC
Jumamosi Mei 14,2016.
Mgambo JKT v JKT Ruvu
Ndanda FC v Yanga SC
Jumapili Mei 15,2016.
Mtibwa Sugar v Simba SC
Kagera Sugar v Stand United
Mwadui FC v Mbeya City
|
No comments:
Post a Comment