KAGAME CUP 2015:-Yanga SC sasa uso kwa Azam FC robo fainali Jumatano July 29, 201 baada ya kushinda leo 1-0 dhidi ya Khartoum N. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, July 26, 2015

KAGAME CUP 2015:-Yanga SC sasa uso kwa Azam FC robo fainali Jumatano July 29, 201 baada ya kushinda leo 1-0 dhidi ya Khartoum N.

Amisi Tambwe akikimbia kushangilia baada ya kuifungia bao pekee Yanga SC dhidi ya Khartoum N ya Sudan leo Julai 26,2015.

RATIBA YA ROBO FAINALI KAGAME 2015   

Jumanne Julai 28, 2015
APR Vs Khartoum N (Saa 8:00 mchana)
Gor Mahia Vs Malakia (Saa 10:00 jioni)
Julai 29, 2015
Al Shandy Vs KCCA (Saa 8:00 mchana)
Azam FC Vs Yanga SC (Saa 10:00 jioni)
Na Mahmoud Zubeiry, DAR ES SALAAM
 
YANGA SC itamenyana na Azam FC katika Robo Fainali ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame Jumatano Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Hiyo inafuatia ushindi wa bao 1-0 jioni ya leo dhidi ya Khartoum N ya Sudan katika mchezo wa mwisho wa Kundi A Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Na kwa matokeo hayo, Yanga SC inamaliza katika nafasi ya pili kwenye kundi hilo kwa pointi zake tisa, baada ya kushinda mechi tatu, zikiwemo dhidi ya KMKM ya Zanzibar 2-0 na Telecom ya Djibouti 3-0.
Bao hilo pekee la Yanga SC leo limefungwa na mshambuliaji wake wa kimataifa wa Burundi, Amisi Joselyn Tambwe dakika ya 30 akimalizia kwa kichwa kona iliyochongwa na Nahodha Haruna Niyonzima kutoka Rwanda dakika ya 30.
Sifa za kipekee zimuendee kipa Ally Mustafa ‘Barthez’ aliyeokoa michomo mingi ya hatari langoni mwake hadi Yanga SC kuulinda ushindi huo. 
Safu ya ulinzi ya Khartoum yenye mabeki warefu ilikuwa kikwazo cha mashambulizi ya mipira mirefu kutoka pembeni ya Yanga, kwani waliicheza kwa wingi na kuiondosha katika hatari.
Yanga SC inamaliza katika nafasi ya pili nyuma ya Gor Mahia ya Kenya yenye pointi 10, wakati Khartoum kwa pointi zake saba inamaliza nafasi ya tatu, ingawa nayo imefuzu Robo Fainali.
Winga wa Yanga SC, Simon Msuva akienda chini baada ya kukwatuliwa na beki wa Khartoum N, Antony Akumu Agay leo. Kulia ni Ahmed Adam.
Mfungaji wa bao pekee la Yanga SC, Amisi Tambwe akiwatoka mabeki wa Khartoum N
Beki wa Yanga SC, Joseph Zuttah akimtoka beki wa Khartoum, Wagdi Awad
Mshambuliaji wa Yanga SC, Malimi Busungu akimtoka beki wa Kahrtoum N, Ahmad Adam

Robo Fainali za kwanza zinatarajiwa kuchezwa Jumanne kati ya APR ya Rwanda na Khartoum N na Gor Mahia na Malakia ya Sudan Kusini, wakati za pili zitachezwa Jumatano kati ya Al Shandy ya Sudan na KCCA ya Uganda na baadaye, Yanga SC na Azam FC zote za Dar es Salaam.
Pata Picha, Habari za Kisiasa, Kijamii, Kiuchumi na Michezo kila stori inayonifikia wakati  wowote ukijiunga na mimi kwa kubonyeza…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad