Utafiti
uliofanywa katika mikoa 13 hapa nchini Tanzania,kuelekea katika uchaguzi mkuu mwezi Octoba 2015, umebaini
kuwa Wananchi wanamhitaji kiongozi ambaye atakuwa na nia thabiti ya kupambana
na kudhibiti rushwa na ufisadi,kutengeneza ajira,kuboresha elimu pamoja na
kuwawezesha wananchi kupata huduma za afya bila bugudha huku matokeo ya
jumla yakionesha kuwa waziri mkuu mstaafu Edward Lowassa ( Pichani ) ndie anayeongoza.
Wakitoa
matokeo ya utafiti kuhusu kutambua vigezo na matarajio ya wananchi katika
kufanya maamuzi ya kuchagua viongozi kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 hapa
nchini uliofanywa na Positive Thinkers Tanzania nakushirikisha viongozi maarufu
wa kisiasa 17 katika mikoa 13,watafiti hao wamesema kero namba moja kwa
wananchi ni rushwa na ufisadi na kwamba wanamhitaji kiongozi mwenye uwezo na
vigezo vya kupambana na kero hiyo na kwamba watafanya uchaguzi kwa kuangalia
uwezo wa kiongozi badala ya itikadi ya vyama vyao.
Aidha
wametoa ushauri kwa tume ya taifa ya uchaguzi kutumia teknolojia ya FAST WEB
APPLICATIONS SYSTEM kwa kuwa mfumo huo unaruhusu kuona bayana hali halisi ya
matokeo ya utafiti mahali popote mtafiti anapoingiza takwimu jambo linaloepusha
malalamiko ya wizi wa kura.
Wameongeza
kuwa kulingana na kura zilizopigwa kuhusu sifa na vigezo vya rais atakayefaa
kigezo cha utendaji kwa vitendo kimechukua nafasi kubwa na kupata kura 1619
sawa na asilimia 49 ya kura zote zilizopigwa na kudhihirisha kuwa rais ajaye
lazima awe na sifa au historia ya utendaji kwa vitendo vinavyodhihirika.
Source:-Itv.
Pata
Picha, Habari za Kisiasa, Kijamii, Kiuchumi na Michezo kila stori inayonifikia wakati wowote ukijiunga na mimi kwa kubonyeza…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia
tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.
|
Sunday, March 29, 2015
Home
SIASA
UTAFIKI KATIKA MIKOA 13 TANZANIA:-Waonyesha Waziri mkuu mstaafu Edward Lowassa anaongoza kuelekea uchaguzi Mkuu 2015.
UTAFIKI KATIKA MIKOA 13 TANZANIA:-Waonyesha Waziri mkuu mstaafu Edward Lowassa anaongoza kuelekea uchaguzi Mkuu 2015.
Tags
# SIASA
Sambaza Hii
Chief Editor | Mhariri
SIASA
Labels:
SIASA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Kuhusu Mwandishi
Journalist / Chief Editor / Tanzanian Blogger
Simu: 0756830214 / 0620197747 / 0789925630.
No comments:
Post a Comment