Rais Jakaya
Kikwete akiongozwa na Naibu Mkurugenzi wa kituo cha televisheni cha Azam TV,
Tido Mhando (kushoto)na msimamizi wa vipindi, Yahya Mohamed wakati wa uzinduzi
wa studio za televisheni hiyo jijini Dar es Salaam jana March 06, 2015. Picha
na Emmanuel Herman.
Rais Jakaya
Kikwete amesema haoni tatizo kwa vyombo vya habari kuandika kashfa zinazoibua
mijadala kwenye jamii kwa kuwa yanasaidia uongozi kujirekebisha, lakini akaonya
kuwa vyombo hivyo vikitumia uhuru wao
kuchochea chuki, vurugu na mifarakano, Serikali haitavumilia.
Rais Kikwete
alikuwa akijibu swali kutoka kwa Tido Mhando wa Azam Media kuwa, anajisikiaje
pale vyombo vya habari vinapoibua kashfa nzito kama za uchotwaji fedha kwenye
akaunti ya escrow na mkataba wa uzalishaji umeme wa Richmond ambazo alisema
zilionekana kutikisa Serikali.
Tido
alimuuliza swali hilo wakati wa mahojiano maalumu kwenye hafla ya uzinduzi wa
studio za kituo cha televisheni cha Azam TV jana March 06,2015.
“Sioni
tatizo,” alisema Rais Kikwete kwenye mahojiano hayo.
Alisema
hachukizwi na habari hizo na hana tatizo na vyombo vya habari, kwani kwa namna
moja au nyingine zinasaidia Serikali yake kujiimarisha na kufanya kazi kwa
weledi zaidi.
“Ukiandika
masuala ya uchochezi, lazima tutakuchukulia hatua, lakini mkiandika kuikosoa
CCM, hilo sina shida nalo,” alisema Rais Kikwete.
Licha ya
kauli hiyo, Rais Kikwete alisisitiza
kuwa, “Tunatakiwa tuwe na uhuru unaozingatia weledi katika utendaji wa
kazi …Serikali haiwezi kuvumilia kuona baadhi ya vyombo vya habari vinatumia uhuru
huo kuchochea chuki, vurugu na mifarakano katika nchi.”
Uzinduzi wa
studio hizo zilizogharimu Dola 31 milioni za Marekani sawa na Sh55 bilioni za
Tanzania, utapanua wigo wa ajira, utafungua ukurasa mpya katika tasnia hiyo na
kwamba italeta chachu ya ushindani kwa vyombo vya habari vingine nchini na
Afrika.SOMA ZAIDI KWA KUBOFYA HAPA..''
|
Saturday, March 07, 2015
UHURU WA HABARI:-JK akana kuyumbishwa na kashfa za Ufisadi.
Tags
# HABARI
Sambaza Hii
Chief Editor | Mhariri
HABARI
Labels:
HABARI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Kuhusu Mwandishi
Journalist / Chief Editor / Tanzanian Blogger
Simu: 0756830214 / 0620197747 / 0789925630.
No comments:
Post a Comment