Mbunge
wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe.
MAHAKAMA Kuu ya Tanzania, leo March 10,2015, imetupilia
mbali shauri lililofunguliwa na Zitto Zubeir Kabwe mwaka jana 2014, akipinga kikao
cha Kamati Kuu ya Chadema kumjadili, kujadili uwanachama wake na cheo chake
ndani ya Chadema, akikitaka chombo hicho cha sheria kwa kuweka zuio la muda,
kusubiri kwanza rufaa yake aliyokuwa amekata katika Baraza Kuu la Chadema.
Mahakama Kuu
iliyoketi chini ya Jaji Richard Mziray, ilikubaliana na hoja za mawakili wa
Chadema waliosema kuwa ufunguaji wa kesi hiyo ulikosewa baadhi ya vifungu vya
sheria na hivyo kumtaka mbunge huyo wa Kigoma Kaskazini kulipa gharama zote za
kesi hiyo.
Zitto hakufika mahakamani badala yake alituma mawakili wake.
Wakati Zitto
akifungua kesi hiyo Januari mwaka jana 2014, tayari Chadema ilikuwa imewafukuza
uanachama Dr. Kitilya Mkumbo na Samson Mwigamba ambao pamoja na Zitto,
walituhumiwa kupanga njama za kufanya mapinduzi ya uongozi ndani ya chama
hicho.
Zitto alikuwa akitetewa na wakili Albert Msando wakati Chadema
iliwakilishwa na Tundu Lissu, Peter Kibatala na John Mallya.
Habari
hii imethibitishwa na Peter Kibatala.
(HABARI:
OJUKU ABRAHAM/GPL).
UNGANA NASI KATIKA FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.
|
Tuesday, March 10, 2015
SHERIA YETU:-CHADEMA Yambwaga Zitto Mahakamani.
Tags
# SIASA
Sambaza Hii
Chief Editor | Mhariri
SIASA
Labels:
SIASA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Kuhusu Mwandishi
Journalist / Chief Editor / Tanzanian Blogger
Simu: 0756830214 / 0620197747 / 0789925630.
No comments:
Post a Comment