Mwili wa
marehemu, Salmin Awadh ukiwekwa kwenye gari ukitolewa kwenye Hospitali ya Mnazi
Mmoja kwenda nyumbani kwake kwa matayarisho ya mazishi.
Mwakilishi
wa jimbo la Magomeni, Zanzibar kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mheshimiwa
Salmin Awadh amefariki dunia ghafla leo akiwa katika Kikao cha Kamati Kuu
Zanzibar, katika ofisi kuu ya chama, Kisiwandui.
Mheshimiwa
Awadh alizaliwa Juni 26 mwaka 1958 na alipata elimu yake ya msingi katika shule
ya Makunduchi na Kiongoni kati ya mwaka 1963-1970.
Marehemu
aliwahi kufanya kazi katika Jeshi la Wananchi wa Tanzania akiwa na cheo cha
Sajenti kati ya mwaka 1976 hadi 1986.
Hadi wakati
mauti yanamkuta alikuwa ni Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Gazeti la Zanzibar Leo,
nafasi aliyokuwa nayo tokea mwaka 2009.
Naibu Katibu Mkuu wa CCM Ndg Vuai Ali amesema marehemu alifika Afisi Kuu
ya CCM Kisiwandui kwa kazi zake na kuhidhuria Kikao cha Sekreteli
kilichofanyika asibuhi hofisini hapo , na kusema marehemu ametoka chumba cha
mkutano na kwenda Afisi kwake ya Mnadhimu wa CCM Baraza la Wawakilishi, ndipo
matatizo yalipojitokeza na kusema anajikia vibaya na kukimbizwa hospitali ya
Rufaa ya Mnazi mmoja kwa matibabu , kufika huko hali ilibandilika na kufariki
dunia.
Marehemu ameacha pigo kwa Chama na wananchi wa jimbo lake.
|
No comments:
Post a Comment