Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Kamishina Msaidizi Mwandamizi wa Polisi
DAVID MISIME – SACP amesema ajali hiyo imehusisha Basi lenye namba za usajili
T. 663 AXL aina ya SCANIA Kampuni ya KIDIA ONE lililokuwa litokea Dar es Salaam
kwenda Mwanza likiendeshwa na ADAM s/o ROBERT, 38yrs, kabila Mnyaturu, mkazi wa
Tegeta Dar es Salaam, liligongana uso kwa uso na Lori namba T.469 CFG Scania
lenye Tellar T. 756 AZX.
Kamanda
MISIME amewataja waliofariki dunia kuwa ni FADHILI S/O HAMIDU SAIDI miaka 36,
Kabila Msukuma ambaye ni dereva wa Lori na utingo wa Bus aliyehafamika kwa jina
la CHOGO S/O CHIGUNDA, miaka 30, Kabila Muha wote wakazi wa Dar es Salaam.
Majeruhi
katika ajali hiyo ni 45 kati yao 34 ni wanaume na 11 ni wanawake; wengine
wametibiwa na kuruhusiwa. Waliolazwa ni 24 kati yao wanaume ni 17 na wanawake
ni 7.
Kamanda
MISIME amesema chanzo cha ajali ni dereva wa Bus Kushindwa kuchukua tahadhali
wakati wa kulipita gari lingine “over take”, na kusababisha ajali hiyo.
Aidha
Kamanda MISIME ametoa wito kwa madereva kuwa na udereva wenye tahadhali
na kuzingatia sheria za usalama barabarani, kwani dereva huyu wa basi
angezingatia hilo ajali hii haingetokea na hatakama ingetokea madhara yake
hayangekua makubwa kiasi hicho.
|
No comments:
Post a Comment