Mbunge wa
Bariadi Magharibi (CCM), Andrew Chenge
akihojiwa kwenye Baraza la Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa
Umma.
Mbunge wa
Bariadi Magharibi (CCM), Andrew Chenge ameibuliwa tuhuma nzito kwenye Baraza la
Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma baada ya kudaiwa kuwa aliishawishi
kampuni ya Independent Power Solution Limited (IPTL) kuingia mkataba na Tanesco
na baadaye kuwa mshauri wa kampuni hiyo binafsi iliyomuingizia Sh1.6 bilioni
zinazohusishwa na sakata la Akaunti ya Tegeta Escrow.
Hata hivyo,
Chenge, ambaye ni mhitimu wa Shahada ya Umahiri wa Sheria kwenye Chuo Kikuu cha
Harvard cha Marekani, aliwasilisha amri ya zuio ya Mahakama Kuu inayokataza
chombo chochote cha Serikali kujadili sakata la escrow hadi hapo shauri
lililopo mahakamani litakapotolewa uamuzi, jambo lililozua mjadala wa kisheria
na kusababisha mwenyekiti wa Baraza la Sekretarieti ya Maadili, Jaji Hamisi
Msumi, kuahirisha hadi leo Februari 26,2015.
Chenge ni
mmoja wa watu kadhaa wanaotarajiwa kuhojiwa na kamati hiyo kutokana na
kuhusishwa na kashfa ya uchotwaji wa zaidi ya Sh.306 bilioni kutoka kwenye
Akaunti ya Tegeta Escrow iliyofunguliwa Benki Kuu kwa makubaliano kati ya
Tanesco (shirika la umeme la umma) na IPTL baada ya pande hizo mbili
kutofautiana kuhusu tozo za malipo ya umeme unaozalishwa na kampuni hiyo
binafsi.
Mwingine ni
mbunge wa Muleba Kusini (CCM), Anna Tibaijuka, aliyekuwa Waziri wa Ardhi,
Nyumba na Maendeleo ya Makazi na ambaye pia aliingiziwa kwenye akaunti yake
Sh1.6 bilioni zinazohusishwa na akaunti hiyo ya escrow.
Wote wawili
waliingiziwa fedha hizo na James Rugemarila, mkurugenzi wa VIP Engineering
iliyokuwa ikimiliki asilimia 30 ya hisa za kampuni ya IPTL.
Tuhuma dhidi ya Chenge
Tangu sakata
la escrow lianze, haikuwahi kuelezwa kuhusika kwa Chenge kwenye sakata hilo.
Lakini jana,
akisoma hati ya malalamiko dhidi ya mbunge huyo wa Bariadi, mwanasheria wa
Sekretarieti ya Maadili, Hassan Mayunga alisema mlalamikiwa, akiwa Mwanasheria
Mkuu wa Serikali (AG) mwaka 1995, aliishauri Serikali kuingia mkataba wa miaka
20 na IPTL wa kuongeza uzalishaji wa umme.
“Mlalamikiwa
baada ya kustaafu wadhifa wa AG, Desemba 24 mwaka 2005, mwaka 2006 aliingia
mkataba wa kuwa mshauri mwelekezi wa kampuni ya VIP Engineering and Marketing
Limited iliyokuwa inamiliki asilimia 30 ya hisa za IPTL,” alisema Mayunga
akikariri hati hiyo ya malalamiko.
“Kitendo cha
mlalamikiwa kuingia mkataba na VIP Engineering and Marketing Limited iliyokuwa
na asilimia 30 ya hisa kwenye kampuni ya IPTL ni ukiukwaji wa fungu la 6 (j) la
Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma ambalo linamzuia kiongozi wa umma
kujinufaisha na utumishi wake uliopita kwa kutumia taarifa alizozipata
alipokuwa anatekeleza majukumu yake kwa manufaa binafsi.
“Kitendo cha
mlalamikiwa kuendelea kuwa mshauri mwelekezi wa kampuni ya VIP Engineering and
Marketing Limited akiwa na wadhifa wa ubunge ni ukiukwaji wa fungu la 6(e) la
Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma ambalo linamzuia kiongozi wa umma kujiingiza
katika mgongano wa maslahi.”
Mwanasheria
huyo aliendelea kusema kuwa mkataba ambao mlalamikiwa aliingia na kampuni ya
VIP Engineering and Marketing Limited ulimpatia manufaa ya kifedha ya Sh1.617
bilioni kinyume na fungu la 12(1)(e) la Sheria ya maadili ya viongozi wa umma.
Aliongeza kuwa mlalamikiwa hakutamka maslahi aliyokuwa nayo katika mkataba wa
Tanesco na IPTL kinyume na fungu 14 la sheria ya Maadili.SOMA ZAIDI HABARI HII KWA KUBOFYA HAPA.
UNGANA NASI KATIKA FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.
|
Thursday, February 26, 2015
SEKRETARIETI YA MAADAILI YA VIONGOZI WA UMMA:- Mazito ya Chenge yaibuka.
Tags
# HABARI
Sambaza Hii
Chief Editor | Mhariri
HABARI
Labels:
HABARI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Kuhusu Mwandishi
Journalist / Chief Editor / Tanzanian Blogger
Simu: 0756830214 / 0620197747 / 0789925630.
No comments:
Post a Comment