Mmiliki wa
nyumba aliyopanga mwalimu huyo, Ruben Shayo aliwaambia Waandishi wa Habari, hapa nchini
kuwa Februari 22 mwaka huu 2015, ulionekana moshi kwenye chumba cha mwalimu huyo,
ambapo wapangaji wengine walimjulisha na kwenda kuushuhudia moshi huo ili
kuweza kujua chanzo chake.
Alisema
baada ya kufika kwenye chumba hicho waliona moshi mwingi ukitokea madirishani
na kufanya juhudi za kuingia ndani ili kuuzima moto huo, ambapo walijaribu
kumuita mwalimu huyo kwa muda mrefu pasipo majibu, lakini mwalimu huyo hakutoka
hadi pale walipomwambia kuwa watakwenda polisi.
Baada ya
kuitikia, ilibidi kumuita mwenyekiti wa mtaa ili waweze kuingia ndani kwake
kuangalia hali ilivyo kwenye chumba chake.
‘’Tuliona funza wakitoka chini ya mlango wake
na harufu mbaya ikitoka na mwenzetu hatujawahi kumuona akioga wala akiingia
chooni ndiyo tukabaini hali hii,’’alisema Shayo.
"tulipoingia ndani tukakutana na nguo
zikiwa zimezagaa na kuonekana kuwa alikuwa akichoma nguo zake”alisema.
Mbali na
hayo pia waliona vyombo mbalimbalia ambavyo vilikuwa vimehifadhiwa kinyesi na
mkojo, huku kukiwa na funza na mende wakiwa wamezagaa hadi kitandani.
Pamoja na
hayo alivitaja baadhi ya vyombo ambavyo alikuwa amehifadhia kinyesi hicho ni
ndoo, sufuria, chupa na mabeseni na harufu kali ya kinyesi ikitapakaa ndani.(Pichani tazama hapa chini)
|
No comments:
Post a Comment