SAKATA LA TEGETA ESCROW TANZANIA:-Watambue kwa Picha Vigogo waliotafuna Mabilioni ya Fedha kutoka Akaunti hiyo - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, November 27, 2014

SAKATA LA TEGETA ESCROW TANZANIA:-Watambue kwa Picha Vigogo waliotafuna Mabilioni ya Fedha kutoka Akaunti hiyo

Viongozi wa Madhehebu ya Dini walioingiziwa fedha na Benki ya Mkombozi ni Askofu Methodius Kilaini shilingi 80.9.

Ndg. Emmanuel Daniel Ole Naiko ambaye alikuwa Mkurugenzi Mkuu wa (TIC) aliingiziwa shilingi milioni 40.4
Mheshimiwa Andrew Chenge Mbunge, ambaye alikuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali na sasa ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti, shilingi Bil. 1.6.
Dr. Enos S. Bukuku ambaye alikuwa Mjumbe wa Bodi ya TANESCO aliingiziwa shilingi milioni 161.7.
Mheshimiwa William Ngeleja Mbunge na ambaye alikuwa Waziri wa Nishati na Madini, shilingi milioni 40.4.
Ndg. Paul Kimiti ambaye ni Mbunge Mstaafu wa Jimbo la Sumbawanga
alipewa shilingi milioni 40.4.
Kwa upande wa Watumishi wa umma,Ndg. Philip Saliboko ambaye alikuwa mtumishi wa RITA aliingiziwa shilingi milioni 40.4
Mhe. Anna Tibaijuka (Mb) na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi shilingi bilioni 1.6.

Mchungaji Alphonce Twimann Ye Simon shilingi milioni 40.4.

Askofu Eusebius Nzigirwa shilingi milioni 40.4

Watu walienda kugawana fedha kwenye Benki tajwa wakiwa na mifuko ya rambo, sandarusi,mabox, magunia na lumbesa Tegeta Escrow

Bilioni 73.5 zilitolewa na kugawanywa kwa watu mbalimbali kinyume cha
Sheria ya Benki Kuu na Taasisi za Fedha ya 2006.

Taarifa ya benki (bank statements) yenye majina na akaunti zote
zilizoingiziwa fedha zimeambatishwa.
Upande wa Majaji Prof. Eudes Ruhangisa, aliingiziwa milioni 404.25 na J.A.K Mujulizi aliingiziwa shilingi milioni 40.4


Kamati imebaini mawasiliano kutoka kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha.

NA HAYA NDIO MAPENDEKEZO YA KAMATI
WAZIRI MKUU MIZENGO PINDA AWAJIBISHWE KWA KUUDANGANYA UMMA WA WATANZANIA - MAPENDEKEZO YA KAMATI YA ZITTO

Filikunjombe: Kamati inashauri kuzitangaza benki za Stanbic na Mkombozi kama asasi za utakatishaji fedha

Filikunjombe: Kamati inashauri bodi ya Tanesco ivunjwe na TAKUKURU iwafungulie mashtaka ya rushwa.

Filikunjombe: Kamati imethibitisha kuwa Naibu waziri wa nishati na madini alisema uongo bungeni naye achukuliwe hatua.

Filikunjombe: Kamati imethibitisha kuwa Waziri wa Nishati na Madini Sospeter Muhongo amekuwa akisema uongo mara nyingi.

Filikunjombe: Kamati pia imethibitisha kuwa Waziri wa nishati na madini ndiye alikuwa dalali mkuu wa kuunganisha hawa watu

Filikunjombe: Kutokana na sababu hizo hapo juu, kamati inapendekeza kuwa Waziri wa Nishati na madini avuliwe madaraka yake.

Kamati inapendekeza kuwa uteuzi wa mwanasheria mkuu wa serikali utengeuliwe mara moja na aadhibishwe maana ametumia vibaya madaraka

Filikunjombe: Kamati pasipo mashaka imejidhihirisha kuwa Waziri mkuu alikuwa akijua jambo hili ila hakuchukua tahadhari.

Filikunjombe: alisema Mwalimu Nyerere kuwa kumbadili Waziri Mkuu sio jambo la ajabu.

Kwa vyovyote vile, Waziri mkuu anapaswa kuwajibishwa kwa namna yoyote ile ili kurudisha heshima ya serikali maana ameudanganya umma wa Watanzania kwa kusema uongo na kuitete kampuni hewa ya PAP isiyokuwepo

Filikunjombe: Kamati yetu inaamini kuwa Bunge hili litaitumia vizuri taarifa yetu hii

Mh. Spika anna Makinda amehairisha shughuli za Bunge na kusema kuwa kesho asubuhi serikali itatoa kauli zake.

Baada ya serikali kutoa kauli zake hapo kesho asubuhi, Wabunge wengine watapata nafasi ya kuchangia.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad