Naibu Spika
wa Bunge, Job Ndugai......Picha ya maktaba yetu.
Hali ni tete. Ndiyo neno ambalo
unaweza kulizungumza kuhusu kashfa ya Akaunti ya Tegeta Escrow.
Mji wa
Dodoma tangu juzi November 21,2014,umejaa pilikapilika zikiambatana na mikutano iliyokuwa
ikijadili kashfa hiyo.
Kamati ya
Uongozi wa Bunge, Kamati ya Uongozi wa Wabunge wa CCM, Baraza la Mawaziri, kwa
nyakati tofauti walikaa kujadili ripoti ya escrow ambayo inatarajiwa kujadiliwa
na Bunge Jumatano na Alhamisi wiki hii.
Leo kikao
cha wabunge wa CCM kinatarajiwa kufanyika kujadili suala hilo.
Wabunge
walionekana kila kona ya Viwanja vya Bunge jana wakijadiliana katika vikundi
kuhusu sakata la escrow, huku wengine wakitaka hata miswada yote iliyobaki
isijadiliwe ili kutoa nafasi kuichambua kwa kina kashfa hiyo.
Wabunge wa
kila vyama wamekuwa wakikutana kuweka misimamo yao kuhusu namna
watakavyoshiriki kujadili ripoti hiyo.
Wabunge wa
CCM wamegawanyika katika makundi matatu; linaloshinikiza waliohusika na wizi
huo wajiuzulu, kundi la watu wasiokuwa na msimamo na kundi linalotaka ripoti
isijadiliwe bungeni.
Kikao cha
Kamati ya Uongozi kilichofanyika jana asubuhi kilikubaliana suala hilo la
escrow lijadiliwe kwa siku mbili badala ya moja iliyokuwa imepangwa awali.
Kamati ya
Uongozi CCM.
Katika kikao
cha Kamati ya Uongozi wa Wabunge wa CCM, wabunge wawili akiwemo Naibu Spika,
Job Ndugai walipewa kibano kuhusiana na matamshi yao kuhusu sakata hilo.
Habari
kutoka ndani ya kikao hicho, zinaeleza kuwa waliokumbana na kibano hicho ni
Mbunge wa Kahama, James Lembeli na Mbunge wa Viti Maalumu, Ester Bulaya, ambao
waliambiwa kwamba matamshi yao wakati wakichangia yalilenga kukifanya chama
hicho kuonekana kuwa ni cha wezi.
“Ndugai yeye
walimbana kwa nini aliruhusu mjadala huo bungeni,” alisema mmoja wa wajumbe wa
kikao hicho.
Aidha,
baadhi ya wabunge wana hofu kuwa mjadala huo huenda usiende bungeni.
|
No comments:
Post a Comment