Nbii wa Kanisa la The Revelation lililopo Buza
Kipera jijini Dar Es Salaam, Yaspi Bendera.
NABII wa Kanisa la The Revelation lililopo Buza Kipera jijini Dar, Yaspi
Bendera amesema uchaguzi mkuu ujao utakuwa balaa kubwa kufuatia maono
anayoyaona wakati akishiriki ibada katika nyakati mbalimbali, Risasi Jumatano
linakupa mkanda kamili.
Akizungumza
wakati wa ibada kanisani kwake na baadaye na waandishi wetu Novemba 16 mwaka
huu, Nabii Yaspi alisema kuna mgongano mkubwa miongoni mwa watu wanaotajwa
kugombea urais, ili kumrithi rais Jakaya Kikwete ambaye alimwelezea kama
kiongozi anayemuona kiroho kila mara.
“Nilimuona
katika maono yangu kama mtu aliye kwenye majaribu makubwa kiroho, nikaandaa
maombi hapa kanisani na tukamuombea kwa muda wa nusu saa na tunashukuru Mungu
hali yake inaendelea vizuri baada ya kufanyiwa upasuaji wa tezi dume nchini
Marekani.
Bado namuona akiwa na maumivu kuanzia sehemu za kiuno, uti wa mgongo
na shingoni mwake.
|
No comments:
Post a Comment