Amiri Jeshi
mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama Rais Jakaya Kikwete akiongozana na
viongozi mbalimbali waandamizi katika serikali ya jamhuri ya muungano na
serikali ya mapinduzi ya Zanzibar na watu maarufu katika kuiaga miili saba ya wanajeshi wa jeshi
la wananchi wa Tanzania waliouwawa nchini Sudan Jumamosi ya July 13 mwaka huu.
Dr Jakaya Mrisho Kikwete. |
Dr Jakaya
Mrisho Kikwete akizungumza katika viwanja vya makao makuu ya jeshi hilo
akionekana dhahiri shairi mwenye majonzi
ikiwa ni muda mfupi mara baada ya kuwaongoza mamia ya waombolezaji
kuiaga miili ya wanajeshi hao waliouwawa na kikundi cha waasi nchini Sudan
katika jimbo la Darfur amesema taarifa za tukio hilo
limemuhuzunisha,kumsikitisha na kumkasirisha na kushauri kuwa wakati umefika wa
kuutazama upya mfumo mzima wa kulinda amani Darfur hasa kuhusu kiwango cha
uwezo wa wanajeshi kujilinda kutokana na ukweli kuwa tayari walinda amani 41
kutoka mataifa mbalimbali wameuwawa na wengine 55 kujeruhiwa.
Aidha waziri
wa ulinzi na jeshi la kujenga taifa Mh Shamsi Vuai Nahodha amekiita kitendo cha
wanajeshi hao wakulinda amani kuuwawa ni dhahiri tendo ovu ambao ni mkakati
maalum wa waasi kutaka kuhakikisha mpango wa umoja wa mataifa katika kuleta
amani katika nchi zenye mifarakano hazifanikiwi huku aliyekuwa naibu katibu
mkuu wa umoja wa mataifa Dr Asha Rose Migiro akisema tukio hilo lisiwakatishe
tamaa katika kupigania amani ya watu wengine katika nchi zenye mifarakano.
No comments:
Post a Comment