Akitoa mada
kuhusu mchango wa vyombo vya dola katika kudumisha amani au kuharibu amani
kwenye kongamano la mustakabali wa amani na usalama wa taifa kwa miaka 50 ijayo
katika chuo kikuu cha Dar es Salaam, mhadhiri wa shule ya sheria ya chuo hicho
bwana Onesmo Kyauke amesema matukio hayo yamejitokeza kutokana na jeshi la
polisi kuzuia maandamano kwa kigezo cha uvunjifu wa amani, wakati wa sheria za
nchi zinaainisha kuwa maandamano ni haki ya kisheria.
Akitoa mada
kuhusu mchango wa siasa na dini katika kudumisha au kuharibu amani,mhadhiri wa
sayansi ya siasa katika chuo kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Bernadetha
Killian tatizo lililopo nchni ni serikali kutimia zaidi njia ya kudhibiti
migogoro badala ya kutatua hali iliyosababisha viongozi wa vyama vya upinzani
kukamatwa na kuachiwa kila wakati ambapo ameshauri kuundwa kwa chombo
chakushughulikia migogoro.
Kwa upande
wake mhadhiri wa chuo kikuu cha Dar es Salaam katika shule ya habari Dokta Ayub
Rioba kuhusu mchango wa vyombo vya habari katika kuimarisha amani na usalama,
amewataka waandishi wa habari kuchagua maoni yakuandika katika kipindi cha
migogoro na kutoa fursa kwa pande zote mbili zisikike kwa namna inayosaidia
jamii kuelewa na kusaidia mgogoro kutatuliwa.
Akifunga
kongamano hilo, waziri wa mambo ya ndani Mhe. Dkt Emmanuel Nchimbi amesema
serikali imekuwa ikichukua hatua za kinidhamu kwa jeshi la polisi ambapo katika
kipindi cha mwaka mmoja zaidi ya askari 102
na maafisa 6 wa jeshi hilo
wamefukuzwa kazi na kesi zao ziko katika mahakama ya kijeshi ambapo kuhusu
maandao amesisitiza swala la kufuata sheria.
Aidha Takwimu
za mashirika ya haki za binadamu zimeonyesha kuwa toka mwaka 2003 hadi 2012
watu 246 wamepoteza maisha kinyume cha sheria nchini Tanzania kutokana na
matukio yanahohusishwa moja kwa moja na Jeshi la Polisi.
No comments:
Post a Comment