Watumishi
walioagizwa kusimamishwa kupisha uchunguzi na ikithibitika wachukuliwe hatua za
kinidhamu kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu ni Bw. Salanga Mahendeka (Mhasibu wa Mapato) ambaye alibainika kuwa na hoja ya mashaka ya fedha zaidi ya
shilingi milioni 276 ikiwa ni pamoja na: Kutosimamia utaratibu wa mapato ya
fedha yaliyoondolewa katika mfumo wa mapato bila idhini ya Afisa Masuuli,
Kusababisha madeni ya wakusanyaji kutotambuliwa kwa kutofanya usuluhishi wa
miamala ya mapato katika mashine za kukusanyia mapato, Kukusanya fedha bila
kuziwasilisha benki.
Mtumishi wa
pili aliyeagizwa Mamlaka ya Nidhamu kumsimamisha kazi ili kupisha TAKUKURU
kufanya uchunguzi juu yake ni Bw.
Emmanuel Maleo (Afisa Ushirika) ambaye alibainika kuchukua
fedha taslimu kwa wafanyabiashara kwa nyakati tofauti mwezi Februari hadi
Machi, 2018 bila kuziwasilisha Benki na kushindwa kuhitimisha mchakato wa
kuwapatia leseni wafanyabiashara hadi Mei, 2018.
Aidha,
Watumishi wengine watano walioagizwa kuchunguzwa na kuchukuliwa hatua za
kinidhamu na Mamlaka zao za Nidhamu kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu
endapo itathibitika tuhuma zao ni za kweli ni pamoja na: Bw. Alexander Bashaula (Mweka Hazina) ambaye ni mkuu wa idara ya
fedha ambaye alifanya uzembe katika kuwasimamia ipasavyo watumishi walioko
chini yake kutekeleza majukumu yao kwa uadilifu pia na kushindwa kumsahuri
ipasavyo Afisa Masuuli kuhusu masuala ya fedha.
Pili ni Bi Beatrice P. Garusya (Afisa Biashara)
ambaye hakutoa leseni za biashara kwa wafanyabiashara waliolipia na kusababisha
malalmiko yasiyo ya lazima kwa wafanyabiashara hao .
Tatu ni Bw. Rogers H. Simkoko (Afisa Tehama)
aliyefanya miamala ya kihasibu badala ya kufanya kazi yake ya ufundi kwenye
mfumo wa kukusanya mapato na kukiuka taratibu kwa kutoa haki kwa Afisa mmoja
kukamilisha miamala peke yake.
Wengine ni Bi Saphina Malimba (Mtunza Fedha)
ambaye hakuwasilisha benki kiasi cha shilingi milioni 32, 098,800/=
alizokusanya kwa kutumia mashine ya kukusanya mapato.
|
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEibmPiIhr9DFhwL8-NKPi49A8IhFJspMHVWIofKbwplGVznxZTic9n4qdg_qAr2BqeAHwYa_8YlTgJSwDy6EicXmkuTEdkf1fkSYwVbzxX6ZBjwinRwCDYdZp9iaWqrSGLJRMNPVsKVW8qT/s640/3.jpg)
![]() |
Mkuu wa Mkoa
Gaguti alimwagiza Mkurugenzi wa
Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo kumrejesha Mtumishi huyo na kumtaka
akabidhi mashine hiyo ifikapo saa 10:00 jioni Agosti 17, 2018 ili usuluhishi
ufanyike na endapo kuna deni atakiwe kulipa mara moja pia alimwagiza Kamanda wa
TAKUKURU Mkoa kufuatilia na kuchukua hatua pia hatua za kinidhamu zichukuliwe
dhidi yake.
Pia Mamlaka ya Nidhamu ya Watumishi wenye madeni hayo iwachukulie hatua za kinidhamu.
Aidha,
vibanda 25 vya Soko la Kabindi vilivyobainishwa kwenye taarifa ya uchunguzi
kuwa havikuwa na mikataba ya kukodishwa Mkuu wa Mkoa Gaguti aliagiza Halmashauri kuandaa mikataba hiyo mara moja
kulingana na bei ya soko ya kukodi vibanda vya biashara kulingana na na
mazingira vilipo pia viboreshwe kwa kuwekewa umeme ili kiwe chanzo cha mapato
cha Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo.
Maamuzi hayo
yalifikiwa na Mkuu wa Mkoa Gaguti
baada ya Katibu Tawala Msaidizi Serikali za Mitaa Sekretarieti ya Mkoa wa
Kagera Bw. David Lyamboko
Kuwasilisha taarifa ya uchunguzi wa awali uliofanyika chini ya uongozi wake
baada ya Katibu Tawala Mkoa kuunda Kamati hiyo na kuipa adidu za rejea ili
kufanya uchunguzi na Kamati hiyo ilianza kazi yake Mei 28, 2018 na kuikamilisha
kazi hiyo Juni 18, 2018.
|
![]() |
Naye Katibu
Tawala wa Mkoa wa kagera CP Diwan Athuman katika kikao hicho maalum
aliwakumbusha wviongozi na Wakuu wa Idara ya Halmashauri ya Wilaya ya
Biharamulo kujitathimini na kujitafakari kama wanamsaidia Mhe. Rais wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe
Maguli kufanikisha adhima ya kuwahudumia wananchi kwa uadilifu.
Pia aliwaasa
watumishi popote walipo katika Halmashauri za Wilaya kujitafakari kwa dhati juu
ya utendajikazi wao, kuwa na mtazamo wa viongozi wa Serikali ya Awamu ya Tano
nini wanakilenga katika kutekeleza majukumu yao, na tatu ni kushirikiana kuwa
na upendo pia na kuwa wakweli.
|
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhNrjLBjHOvJJLLNZdlJhgaKdb3sGT7UjD1mNqCzYM-T08Fs4BpqzNWSELCMjcQhyeINViLe7s6sy7BzLjtScPQ_h97J-TVZRLXeAB6uZViqWfWsS8eColuc08uAoBBl6djVpC_iI6u2v7o/s640/6.jpg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhCMGp14siEeIYyqrU-42wEizuNETdmESFvuamDGyur6s8Baf7eDLlSbjk-xlrsLmp4EZLT1GnWCyYs5FCYL3wRSXgqN1ELpPatA8i5U3vFhxBUy7YQjX3zuxivtTFy47hZ2nM2NTquAXG-/s640/7.jpg)
No comments:
Post a Comment