Wenyeji Geita Washindwa Kutamba Mechi Ligi ya Mabingwa wa Mikoa. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Friday, May 11, 2018

Wenyeji Geita Washindwa Kutamba Mechi Ligi ya Mabingwa wa Mikoa.

MATOKEO YA MECHI ZA LEO MAY 11, 2018.

Wenyeji GIPCO FC  Mabingwa wa soka mkoani Geita wameshindwa tena leo May 11, 2018 kuibuka na ushindi kwenye uwanja wa nyumbani wa WAJA wakati timu hiyo iliposhukda katika dimba hilo kucheza mechi yake ya 3 ya ligi ya Mabingwa wa Mikoa dhidi ya UNGINDONI FC ya Dar es Salaam.

Mchezo huo wa kundi A umemalizika kwa sare ya bila kufungana huku Mabingwa wa Soka mkoa wa Mwanza PHANTOM FC wakiishindilia bao 2-1 NYAMONGO FC ya Mara kwenye mchezo wa mapema kabisa saa 8 mchana.

Kwa matokeo hayo ,PHANTOM FC wanaongoza kundi hilo wakiwa na Point 7 za michezo 3 wakifuatiwa na KUMUYANGE FC walioshinda jana bao 3-2 dhidi ya AMBASSADOR  FC ya Simiyu –wakijikusanyia point 6 za mechi 2.

KATIKA KITUO CHA RUKWA.

Mabingwa wa soka mkoa wa Kigoma-RED STARS wameibuka na suhindi wa bao 1-0 dhidi ya LAELA FC ya Rukwa katika mchezo wao wa pili wa Ligi ya Mabingwa wa Mikoa.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad