Simba SC Bingwa Ligi Kuu Tanzania. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Friday, May 11, 2018

Simba SC Bingwa Ligi Kuu Tanzania.

Simba SC.

Kipigo cha 2-0 ilichochezea Yanga SC kutoka kwa Tanzania Prisons, kimeivua rasmi Ubingwa wa VPL iliyoubeba msimu wa 2016/2017 ambao sasa unakwenda mitaa ya Msimbazi kwa Simba SC ambayo hata ikipoteza mechi zake zote (3) bado hakuna timu ambayo itaweza kuifikia.

Simba SC inaongoza Ligi msimu huu 2017/2018 ikiwa na pointi 65 baada ya kucheza mechi 27, imebakiza mechi tatu kabla ya msimu wa ligi haujaisha. 

Yanga SC ambayo ilikuwa Bingwa mtetezi inaendelea kubaki na pointi zake 48 baada ya kuheza mechi 25 na kubakiza mihezo mitano (5).

Endapo Yanga SC itashinda michezo yote mitano iliyosalia itafikisha pointi 63, ambazo ni pointi mbili nyuma ya Simba SC.

Ubingwa wa VPL 2017/2018 utaipa Simba SC kombe, fedha taslimu lakini pia wataiwakilisha Tanzania katika mashindano ya kombe la vilabu Bingwa Afrika msimu ujao 2018/2019 mashindano ambayo walicheza mara ya mwisho msimu wa 2012/2013.
Yanga SC.

Matokeo haya pia yanamaanisha Yanga CS hawatashiriki michuano ya Afrika mwakani, kwani tayari wametolewa pia na kwenye Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), maarufu kama Azam Sports Federation (ASFC) katika hatua ya Robo Fainali tu.  

Mechi nyingine ya Ligi Kuu May 11,2018, bao pekee la Vincent Philipo dakika ya 45 na ushei limeipa Mbao FC ushindi wa 1-0 dhidi ya Ndanda FC Uwanja wa CCM Kirumba mjiniu Mwanza.

Kwa ushindi huo, Mbao FC inafikisha pointi 27 baada ya kucheza mechi 27 na kupanda kwa nafasi moja hadi ya 13, wakati Ndanda FC inabaki nafasi ya 15 kwa pointi zake 23 za mechi 28 kwenye Ligi ya timu 16, ambayo timu mbili zitashuka wiki mbili zijazo. 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad